WANAHARAKATI WALIA NA WALEMAVU, WATAKA UCHAGUZI WA MABARAZA YA KATIBA URUDIWE

Washirika wa jukwaa la wazi la semina za jinsia na maendeleo GDSS linalo ratibiwa na TGNP, hii leo wameitaka serikali kurudia uchaguzi wa wajumbe wa mabaraza ya katiba ya wilaya, kata na mitaa

Tamko hilo limekuja baada ya taasisi hiyo kueleza kuwa mchakato huo uligubikwa na Ubaguzi wa kijinsia, Rushwa, Udini, na siasa huku miongoni mwa watu 7 watakao wakilisha mitaa hakuna nafasi ya walemavu

Akitoa tamko hilo mbele ya waandishi wa habari hii leo TGNP, katibu wa GDSS bwana Badi Darusi amesema kuwa nilazima Serikali kurudia mchakato huo ilimakundi yaliyo achwa pembezoni kama walemavu na wanahabari wapewe nafasi

“Hakuna anaye wakilisha walemavu, watu 7 ambao ni wanawake 2 wasichana 2, wanaume 2 na wengine 1 hakuna mlemavu...walemavu hawana mwakilishi mabaraza ya katiba” alisema Darus

Darus amesema, katika swala la Siasa kuchukua nafasi kubwa. Vyama vya siasa vilikuwa zinatumia fursa ya kufanya kampeni chafu kinyume nataratibu zilizo wekwa na Tume ya taifa ya mabadiliko ya katiba.

Aidha wameelezea kuwa mchakato huo pia uligubikwa na vitendo vya ubaguzi na unyanyasaji uliofanywa na baadhi ya viongozi wa mitaa na vyama vya siasa hali iliyopelekea kutoa tamko lao hivyo kuitaka serikali kurudia tena zoezi la uchaguzi wa mabaraza ya katiba.


EmoticonEmoticon