UWAKILISHI KWENYE MKUTANO MKUU TFF, HUKU LIGI KUU YAINGIA RAUNDI YA NNE

UWAKILISHI KWENYE MKUTANO MKUU TFF, HUKU LIGI KUU YAINGIA RAUNDI YA NNE


UWAKILISHI KWENYE MKUTANO MKUU TFF

Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imesema uwakilishi wa ujumbe kwenye Mkutano Mkuu unaanzia kwenye chama cha mpira wa miguu cha mkoa, kufuatiwa na chama shiriki na baadaye klabu ya Ligi Kuu.
 
Mwongozo huo juu ya uwakilishi wa wajumbe kwenye Mkutano Mkuu umetolewa kutokana na maombi ya Sekretarieti ya TFF kwa kamati hiyo iliyokutana jana (Septemba 16 mwaka huu) baada ya kubaini baadhi ya wajumbe wanashikilia nafasi mbili kwenye vyama tofauti.
 
Kwa mujibu wa Ibara ya 5 ya Katiba, kuna makundi ya aina tatu ya wanachama wanaounda TFF. Makundi hayo ni vyama vya mikoa, vyama shiriki na klabu za Ligi Kuu.
 
Sekretarieti ya TFF imebaini kuwa kuna baadhi ya viongozi wa kuchaguliwa wa mikoa ambao pia ni viongozi wa vyama shiriki na klabu za Ligi Kuu, hivyo wana nafasi zaidi ya moja ya kuingia kwenye Mkutano Mkuu. 

HUDUMA ZA AFYA BADO KIKWAZO CHA KUPUNGUZA VIFO VYA MAMA NA MTOTO


Baadhi ya wilaya hapa nchini bado zinakabiliwa na ukosefu mkubwa wa mahitaji ya huduma za afya kama vile ukosefu wa madawa, madaktari pamoja na vifaa vya matibabu kituambacho kinarudisha nyuma juhudi za kupambana na vifo vya mama na mtoto hapa nchini

Hayo yamebainishwa leo katika mkutano uliokuwa unajadili maendeleo ya mradi wa kuboresha afya,


Ya watoto walio chini ya miaka 5 na akina mama wajawazito unaotekelezwa katika wilaya za Same, Kilindi na Arusha vijijini chini ya shirika la World Vision.
ZOEZI LA KUONDOA WA HAMIAJI HARAMU HALINA UPENDELEO

ZOEZI LA KUONDOA WA HAMIAJI HARAMU HALINA UPENDELEO



Wizara ya mambo ya ndani nchini Tanzania imetoa ufafanuzi juu ya tuhuma kadhaa za uonevu na upendeleo, kuhusiana na zoezi linaloendelea hivi sasa la kuondoa wahamiaji haramu katika maeneo mbali mbali hapa nchini


Hii leo Blog hii ilishuhudia raia wa nchi mbalimbali miongoni mwao walikuwepo wamalawi zaidi ya 1500, wa Nigeria na nchi zingine wakijiandikisha katika ofisi za uhamiaji jijini Dar es salaam ili waweze kutambulika kisheria
KESI DHIDI YA PINDA NA KAULI YA PIGA TU, WALALAMIKAJI WAAMBIWA HAWANA HAKI YA KUSHITAKI

KESI DHIDI YA PINDA NA KAULI YA PIGA TU, WALALAMIKAJI WAAMBIWA HAWANA HAKI YA KUSHITAKI



Mahakama kuu ya Tanzania hii leo imetoa siku 14 hadi Octoba 18 mwaka huu kwa kituo cha sheria na haki za binadamau LHRC na chama cha wanasheria wa Tanganyika TLS 



kujibu hoja za serikali waliofungua didhi ya Waziri mkuu Mizengo Pinda.

Katika shauri hilo, kituo cha sheria na haki za binadamu na chama cha wanasheria wa Tanganyika kwa pamoja wanaitaka mahakama kuu itamke kuwa waziri mkuu alivunja katiba na kumtaka Waziri mkuu Mizengo Pinda afute kauli aliyoitoa bungeni ya kuvitaka vyombo vya dola vipige wananchi
CHAMA CHA WALIMU CHAZIDI KULIA NA SERIKALI JUU YA MADAI YAO

CHAMA CHA WALIMU CHAZIDI KULIA NA SERIKALI JUU YA MADAI YAO

Mwenyekiti wa chama cha waalimu nchini bwana Gratius Mukoba ameitaka serikali kuwalipa walimu madai yao yanayofikia kiasi cha shilingi Billioni 40 hivi sasa ili kuwepo na utekelezaji mzuri wa mpango wa maendeleo makubwa sasa katika sekta ya elimu nchini.

Akiongea na waandishi wa habari hii leo jijini Dar es salaam, bwana Mukoba amesema wanategemea madai yao kushugulikiwa mapema kabla ya kikao hicho na kuongeza kuwa matarajio ya waalimu wote nchini ni kuona madai hayo yanapatiwa ufumbuzi.
MAONYESHO YA BIDHAA ZA WACHINA YA FUNGULIWA

MAONYESHO YA BIDHAA ZA WACHINA YA FUNGULIWA


 Waziri mkuu wa Tanzania Mhe. Mizengo Pinda hii leo amefungua maonyesho ya bidhaa za wachina kwa nchi za Afrika yanayofanyika jijini Dar Es Salaam kwa siku tatu yakiwa na lengo la kubadilishana ujuzi wa kutengeneza bidhaa mbali mbali na kuwapa uwezo wazalishaji katika nchi za afrika.

Akiongea katika ufunguzi huo, Mhe. Pinda amewataka wafanyabiashara hasa wa Tanzania kutumia vizuri fursa hii ili kuendeleza uchumi na kupanua wigo wa biashara ndani na nje ya Nchi.

CHAMA CHA WALIMU CHAZIDI KULIA NA SERIKALI JUU YA MADAI YAO

CHAMA CHA WALIMU CHAZIDI KULIA NA SERIKALI JUU YA MADAI YAO


Mwenyekiti wa chama cha waalimu nchini bwana Gratius Mukoba ameitaka serikali kuwalipa walimu madai yao yanayofikia kiasi cha shilingi Billioni 40 hivi sasa ili kuwepo na utekelezaji mzuri wa mpango wa maendeleo makubwa sasa katika sekta ya elimu nchini

Akiongea na waandishi wa habari hii leo jijini Dar es salaam, bwana Mukoba amesema wanategemea madai yao kushugulikiwa mapema kabla ya kikao hicho na kuongeza kuwa matarajio ya waalimu wote nchini ni kuona madai hayo yanapatiwa ufumbuzi.
KAGAME NA JK USO KWA USO KUMALIZA MZIZI WA FITNA

KAGAME NA JK USO KWA USO KUMALIZA MZIZI WA FITNA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete leo, Alhamisi, Septemba 5, 2013, amekutana kwa faragha na Rais wa Rwanda, Mheshimiwa Paul Kagame katika mazungumzo yaliyokwenda vizuri na kuwaridhisha viongozi hao wawili wa nchi jirani.

Viongozi hao wamekutana kwa saa moja katika mkutano uliofanyika kwenye Hoteli ya Munyonyo Commonwealth Resort, nje kidogo ya mji wa Kampala, Uganda.
WANANCHI WATAKIWA KUTOA MAONI MPANGO WA OGP

WANANCHI WATAKIWA KUTOA MAONI MPANGO WA OGP


MWALIKO KWA WADAU KUCHANGIA MAONI KATIKA ZOEZI LA SERIKALI
KUJITATHMINI (SELF ASSESSMENT) KATIKA UTEKELEZAJI WA
MPANGO WA UENDESHAJI SHUGHULI ZA SERIKALI KWA
UWAZI (OPEN GOVERNMENT PARTNERSHIP)


Serikali kwa kushirikiana na Asasi za Kiraia (Civil Society Organizations) inatakiwa kufanya zoezi la tathmini (Self Assessment) ili kujua ni kwa kiwango gani ahadi zilizoainishwa katika mpango wa OGP zimetekelezwa.

Kategori

Kategori