HUDUMA ZA AFYA BADO KIKWAZO CHA KUPUNGUZA VIFO VYA MAMA NA MTOTO


Baadhi ya wilaya hapa nchini bado zinakabiliwa na ukosefu mkubwa wa mahitaji ya huduma za afya kama vile ukosefu wa madawa, madaktari pamoja na vifaa vya matibabu kituambacho kinarudisha nyuma juhudi za kupambana na vifo vya mama na mtoto hapa nchini

Hayo yamebainishwa leo katika mkutano uliokuwa unajadili maendeleo ya mradi wa kuboresha afya,


Ya watoto walio chini ya miaka 5 na akina mama wajawazito unaotekelezwa katika wilaya za Same, Kilindi na Arusha vijijini chini ya shirika la World Vision.

Mganga mkuu wa wilaya ya Kilindi Dkt Abbas Mungia, amesema wilaya yake inaukosefu mkubwa wa wakunga, madawa na wakati mwingine yale yanayo patikana yapo chini ya viwango vya wizara ya afya ambavyo vinataka viwepo katika maeneo ya Wilaya, kata na vitongoji

Aidha amratibu wa masuala ya Afya katika shirika la World Vision bi. Agnes Victor amesema shirika hilo linahakikisha vifo vyao mama na mtoto vinapungua kufikia kwa asilimia 93% ifikapo mwaka 2015.

Wizara ya Afya hapa nchini pamoja na mashirika mbalimbali ya Afya yanafanya juhudi ilikuweza kupunguza vifo vya mama na mtoto ambavyo vinatokea kutokana na sababu mbalimbali, ikiwemo kina mama kutohudhuria kliniki, kuto jifungua katika vituo vya afya, huduma mbovu za afya pamoja na upungufu wa wauguzi.


EmoticonEmoticon