NANI MWENYE HAKI YA KUSHIKA SIMU YA MPENZI WAKE?? KATI YA HAWA WAWILI??

Kundi la kwanza ni ~ Wanandoa ambao tayari ni mume na mke au wanaishi pamoja kama wanafamilia.

Kundi la Pili ni ~ Walio kwenye Uchumba ambao hawaishi pamoja au hawaja oana lakini wanatarajia kuingia katika ndoa.

                  Swali langu katiya makundi hayo mawili ni kundi lipi linauhalali wa kuwa huru na simu ya mkononi ya mpenzi wake, bila kujali kama ni mwana mke au mwanaume.

Swala la simu miongoni mwa wapenzi huwa lina utata na matatizo mengi, Campasvision imefanya utafiti katiya makundi hayo mawili kwa kuuliza maswali baada ya kubaini kuwa kuna kundi moja linaamini lina uhalali wa kuwa huru na simu ya mpenzi wake, huku kundi lingine likidai akuna uhalali wakuwa huru na simu ya mpenzi wako kwa sababu tofauti tofauti ambazo walizitaja 

Tukianza na kundi la kwanza ambalo kila mtu anamtegemea mwenzake, yani mume na mke kwani nikama familia au umoja wenye mambo mengi yanayo fanyika kwa pamoja na kuwa jumuisha pamoja, tusema nifamilia pengine yaweza kuwa na watoto au lah.

Wengi wa watu niliofanya nao mahojiano katika kundi hili ambao wote walikuwa walio oa na kuolewa, kundi hili walisisitiza juu ya kuwa huru na simu ya mwenza wako kwa sababu nyingi na zilizo kuwa na msingi kabisaa, 

Hakuna aliye kuwa na sababu ya kwa nini mke wake au mume wake asishike simu yake, aidha kwa idhini au bila idhini kutokana na kuwa tayari wao nifamilia moja mipaka kama hiyo aijengi familia. Na endapo kutakuwa na mtu anamkatazia mke au mume wake kushika simu yake ya mkononi basi siyo mwaminifu katika mapenzi yake na kwakuwa simu ndio mficha siri zetu basi wengi wanahofia kuumbuka, ilikuji ficha basi anaamua kuwa mkali kwenye simu yake.

Kundi la Pili ni la wale wachumba ambao wanatarajia kuingia katika ndoa, ila bado kila mtu anakaa peke yake au anakaa na wazazi wake. majibu niliyo pata toka kwenye kundi hili kwa wasichana na wavulana halikuwa la moja kwa moja, kwamba ninani mwenye uhalali wa kushika simu ya mwenza wake kati ya kundi la kwanza au kundi la pili

Wengi wa kundi hili waliwajibia waliokwenye ndoa kuwa ndio wanastahili kushika simu ya mwenziwake. Lakini miongoni mwao hawakuwa tayari kusema kama wanaona uhalali wa kushika simu za wapenzi wao, na hawa walikuwa wasichana kwa wavulana ambao bado wako kwenye uchumba

Nilicho kibaini ambao ni utofauti wa makundi haya mawili nikwamba, Kundi la kwanza tayari limeshajiwekea malengo na uhakika wa mahusiano yao lakini kundi la Pili bado hawana msimamo na malengo kwenye mahusiaono yao ndio maana wakashindwa kutoa jibu la moja kwa moja, na swala la kushika simu za wapenzi wao au mpenzi kushika simu yake ilikuwa kasumba kubwa naamini bado hawajawa waaminifu na msimamo wa mahusiano yao

Kitu cha msingi ambacho kila mtu anatakiwa kujua anapokuwa katika mahusiano, nijukumu la kulinda penzi na kuwajibika kwa mwenza wake bila kujali wewe ni mume/mke au wewe ni mchumba tu, kwani hakuna anaye ingia katika maisha ya ndoa bila kuanzia katika uchumba.

Kwa mtu ambaye ni mwaminifu hakuna sababu ya wewe kuficha simu au kuzima simu hata kuweka password na vikwazo vingine ambavyo vinapelekea kuweka mipaka kati ya wapenzi wetu, kumbuka kwamba kuwa muwazi katika mambo yako hujenga mahusianao na kuleta uaminifu kati yenu.

kulingana na mada yetu hakuna asiye kuwa na uhalali wakushika simu ya mwenzi wake kama tayari umeamua kuwa huyu ni wangu wa maisha, hasa kwa wale walioko kwenye ndoa. si vyema kumkataza mwenza wako kushika simu yako na kama hili nitatizo ambalo unahisi linakukera sana pale mpenzi wako anaposhika simu yako au pale anapokukataza kushika simu yake. kila kitu kina sababu na maana yake ni bora kuzungumza ilikuweka mambo sawa 

Kikubwa cha kufanya nikupunguza mabavu na maamuzi ambayo yanaegemea upande wako bila kujali mwenzako anajisikiaje au atanielewaje katika hili swala... kuwajibika katika kulinda mahusiano kwa kila namna ni jukumu la kila mmoja wenu. Tuwe watu wakuweka vitu wazi na kusisitiza uhaminifu miongoni mwenu

HAPA KAZI TUU.... JOHN POMBE MAGUFULI AANZA NA WIZARA YA FEDHA

HAPA KAZI TUU.... JOHN POMBE MAGUFULI AANZA NA WIZARA YA FEDHA


Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli hii leo amefanya ziara ya kushtukiza katika ofisi za Wizara ya fedha na kukuta baadhi ya watendaji katika Wizara hiyo wakiwa hapo ofisini Ikiwa bado ni muda wakazi.

Katika hali isiyoyakawaida, Rais Magufuli pia alitembea kwa miguu akitokea Ikulu kwenda ofisini hapo akiambatana na walinzi wake ambapo alikuta maofisa hao wakiwa awapo kazini.



Watanzania mbalimbali wametoa maoni kwa njia ya mitandao ya kijaa  juu ya ziara hiyo ya kushtukiza kuwa ya kuimarisha uchapakazi kwani viongozi wengi wa serikali wamekuwa wakifanya kazi kimazoea jambo ambalo linapelekea maendeleo kurudi nyuma.

Hivyo kumtaka Mhe Rais JP kuhakikisha kuwa anafanya ziara za mara kwa mara ili aweze kuwawajibisha wafanyakazi wazembe serikalini.

JANET MBENE WASHUKURU WANANCHI WA JIMBO LA SONGWE KWA KUMPA KURA ZA KISHINDO


 MBUNGE mteule katika Jimbo la Ileje mkoani Songwe ambaye pia ni Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Janet Mbene (CCM) amewashukuru wananchi wa jimbo hilo kwa kumpa kura za kishindo, madiwani na  Dkt. Jonh
Magufuli anayewania urais.

Akizungumza na wakazi wa Ileje, Mbene alisema ushindi wa kura 27,583 aliopewa na wana Ileje dhidi ya Emmanuel Mbuba wa NCCR Mageuzi aliyepata kura 14,578

atahakikisha anawapa wananchi hao kupitia ushirikiano, usimamizi na utatuzi wa changamoto mbalimbali
zinazowakalibi.

“Awali ya yote niwashukuru wana Ileje kwa kuonesha imani kubwa kwangu, madiwani na mgombea urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dkt. Jonh Magufuli. Wana Ileje wametupa kura za kishindo nami ninawahaidi sitawaangusha katika utekelezaji wa ahadi nilizozitoa kwenu wakati wa kampeni,” 
alisema Mbene.

CD ZISIZO NA CHATA YA TRA KUPIGWA STOP JULY MOSI

Baraza la sanaa Tanzania kwa kushirikiana na Baraza la hatimiliki nchini zimejipanga kuzuia mauzo ya CD za wasanii wa bongo ambazo hazina chata ya Mamlaka ya mapato Tanzania (TRA), ili kuongeza kipato cha wasanii na Taifa kwa ujumla.

Wakiongea na Blog hii leo Dar es salaam, Kaimu katibu mtendaji wa BASATA bwana Godfrey Lebejo na Mtaalamu wa Tehama kutoka COSOTA wamesema zoezi hilo litaanza rasmi July 1 mwaka huu.

Kwa muda sasa wasanii wa bongo wamekuwa wakilalamika kuibiwa kazi zao, hivyo mamlaka hizi zimeamua kutumia mbinu mpya ya kudhibiti kazi hizo kwa lengo la kuinua maslahi ya wasanii.

TUME YA UCHAGUZI ZANZIBAR (ZEC) IMEFUTA MATOKEO YA UCHAGUZI

Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi zanzibar salim jecha salim ametangaza kufutilia mbali matokeo ya uchaguzi visiwani humo kwa madai kuwa kumekuwepo kwa kura nyingi kuliko idadi iliyopo kwenye daftari la wapiga kura.
Akitangaza suala hilo mwenyekiti wa zec amesema kumetokea kuwepo kwa dosari nyingi kwenye upigaji kura jambo ambalo amelitaja kuwa sio wa haki.
"Kumegundulika kasoro nyingi katika uchaguzi huu miongoni mwa hizo ni kubainika kwa baadhi ya vituo vimekuwa na kura nyingi kuliko daftari la wapiga kura wa kituo husika." amesema salim jecha
Amesema hilo ni jambo la kushangaza ikizingatiwa kwamba "baadhi ya wapiga kura hawakwenda kuchukuwa vitambulisho vyao vya kupigia kura".

WATU WANNE WAKAMATWA KWA KUNUNUA KADI YA MPIGA KURA MOROGORO



Ikiwa imebaki siku chache kuelekea uchaguzi mkuu katika hali isiyo ya kawaida watu wanne wasiofahamika itikadi zao za kisiasa  wamekamatwa na wafuasi wa chama cha demokrasia na maendeleo(chadema) kwa madai ya kupita katika kata za manispaa ya morogoro na kudai shahada za wapiga kura kwa nguvu na kuanza kuorodhesha majina ya wananchi na namba zao za simu




kwa upande  wananchi mashuhududa   waliokumbana na watu hao  katika harakati za  kuwaandikisha  wapiga kura majina  wameeleza jinsi watu hao walivyokuwa wakifanya zoezi hilo  kwa kudai kwa lazima shahada za kupigia kura ambapo baadhi ya watu  walikubali na wengine wafikisha  jambo hilo kwa afisa mtendaji wakata na wananchi waliamua kuungana na kuwakamata na kisha kuwapeleka katika kituo cha polisi cha mji wa morogoro.

MHE. DEO FILIKUNJOMBE AFARIKI DUNIA KWA AJALI YA NDEGE



Aliyekuwa mgombea ubunge wa jimbo la ludewa kupitia tiketi ya chama cha mapinduzi ccm mhe. deo filikunjombe na wengine watatu wamefariki dunia katika ajali ya chopa iliyotokea eneo la hifadhi ya selous

Akidhibitisha kutokea kwa ajali hiyo kamishna wa operesheni na mafunzo wa jeshi la polisi poul chagonja amesema ndege hiyo ilikuwa imebeba abiria wanne wakitokea dar es salaam kuelekea njombe na waliotambuliwa mpaka sasa ni rubani wa ndege hiyo capten willium silaa na deo filikunjombe

Kamishna chagonja amesema jeshio la polisi limaendelea na uchunguzi wa ajali ya ndege hiyo yenye namba za usajili 5Y DKK unaendelea na kuwa abiria wengine wawili bado hawajatambuliwa kwa majina yao.
sauti ya kamishna chagonja akielezea zaidi

BUNGE LAVURUGIKA NA KUAHIRISHWA , KAULI YA WAZIRI MKUU MHE. PINDA YASUBIRIWA KWA HAMU



Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo asubuhi amelazimika kusitisha shughuli za bunge baada ya wabunge kutaka serikali kuahirisha mchakato wa kura ya maoni pamoja na kutoa taarifa ya uandikishwaji wa wapigakura kwa kutumia mfumo wa kielektroniki wa BVR.




Wakichangia hoja bungeni Mbunge wa Kisarawe Mh. Suleiman Jaffo na Mbunge wa Ubungo Mh. John mnyika wametaka suala hilo lijadiliwe kama dharura na kutolewa majibu na serikali kuhusu hatama ya mchakato huo.

Taharuki ilizuka baada ya Spika wa Bunge hilo Mhe. Makinda kutaka kuzitupilia mbali hoja hizo. Wabunge walianza kupiga kelele kutaka majibu ya serikali papo hapo na ndipo Spika wa bunge alilazimika kuhairisha kikao hicho mpaka jioni ambapo leo ni kikao cha mwisho cha bunge hilo.

Mnyika “ Nimesimama kupata Idhini kwa mujibu wa kanuni kuomba shuguli za mbunge zisitishwe na badala yake tujadili zoezi la uandikishwaji kwani mpaka sasa zoezi halijakamalika hata kwa mkoa mmoja, hivyo Waziri mkuu kwakuwa yupo hapa Bungeni atupe majibu nini kinaendelea” Amesema Mnyika

Spika “Hoja hii na ile ya kwanza zinafanana, majibu mtajibiwa baadae katika kikao cha jioni” Alisema spika. Aidha wabunge wa Upinzani walionesha nia ya kutaka kujua hivyo kupiga kelele kwakusema “Tuna taka Majibu” hali iliyopelekea spika wa bunge kuahirisha Bunge hadi jioni.
MABADILIKO YA MAKAMANDA WA POLISI WA MIKOA

MABADILIKO YA MAKAMANDA WA POLISI WA MIKOA

TAARIFA YA JESHI LA POLISI KWA VYOMBO VYA HABARI



Inspekta Jenerali wa Polisi IGP Ernest Mangu amefanya mabadiliko kwa baadhi ya makamanda wa polisi wa mikoa.

Miongoni mwa makamanda wa mikoa waliofanyiwa mabadiliko ni pamoja na aliyekuwa kamanda wa Mkoa wa Simiyu, Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Charles Mkumbo anakwenda kuwa kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza na nafasi yake kuchukuliwa na aliyekuwa afisa mnadhimu mkoa wa Manyara Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Gemini Mushi. Aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Valentino Mlowola anakwenda kuwa Kaimu Kamishna wa Intelijensia makao makuu.

Aliyekuwa kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Maria Nzuki amehamishwa makao makuu kuwa mkuu wa polisi jamii na nafasi yake kuchukuliwa na aliyekuwa kamanda wa kikosi cha ufundi Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Lucas Mkondya.

Wengine ni aliyekuwa Kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Godfrey Kamwela amehamishiwa Polisi Makao Makuu na nafasi yake kuchukuliwa na aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Njombe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Fulgence Ngonjani.

Aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Ulrich Matei amehamishiwa Kanda Maalum ya Dar es Salaam kuwa mkuu wa utawala na nafasi yake kuchukuliwa na aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kigoma Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Jafary Mohamed.

JIHADHARI NA MATAPELI AJIRA ZA WALIMU WAPYA 2016, SOMA HAPA

                           
                                             


JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU AJIRA YA WALIMU WAPYA WA
SHULE ZA MSINGI, SEKONDARI NA VYUO VYA UALIMU
MWAKA 2015/16.




 JIHADHARI NA MATAPELI

Kumekuwepo na Tangazo la upotoshaji kuhusu Ajira ya walimu wapya kwa mwaka 2015/16 (TANGAZO No. T.022/15TMS 2015) linalodaiwa kuwa limetolewa na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi na kusambazwa kwenye Mitandao ya Kijamii. Taarifa zilizotolewa katika tangazo hilo siyo za kweli na Wizara haihusiki nazo.

Aidha, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi inapenda kuufahamisha umma kuwa ajira ya Walimu wa ngazi ya Cheti, Stashahada, na Shahada hufanywa na Ofisi ya Waziri Mkuu - TAMISEMI baada ya kupata kibali cha Ajira kutoka Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma. Hivyo Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi haihusiki moja kwa moja na zoezi hilo.

Kutokana na mgawanyo wa majukumu ya Wizara mbalimbali, taarifa sahihi kuhusu ajira mpya za walimu kwa mwaka huu wa fedha zitatangazwa na Mamlaka inayohusika yaani Ofisi ya Waziri Mkuu - TAMISEMI mara watakapokamilisha taratibu zinazotakiwa.


Imetolewa na:
Katibu Mkuu,
WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI
23 Machi, 2015


 TCRA YATOA MAAGIZO KWA MAKAMPUNI YA SIMU JUU YA TOZO ZA VIFURUSHI VYA MAZUNGUMZO, MESEJI NA INTANETI

TCRA YATOA MAAGIZO KWA MAKAMPUNI YA SIMU JUU YA TOZO ZA VIFURUSHI VYA MAZUNGUMZO, MESEJI NA INTANETI


KUHUSU TOZO KWENYE SEKTA YA TEHAMA

Katika wiki ya pili ya Februari 2015, baadhi ya watoa huduma za mawasiliano ya simu za mkononi walianzisha vifurushi vya mawasiliano na bei na kusabababisha malalamiko kutoka kwa watumiaji na umma kwa ujumla. TCRA, kwa kuzingatia upeo wa shughuli zake, imechambua hali hiyo na inapenda kutoa maelezo na maagizo ambayo yatawezesha kuondoa sintofahamu iliyopo na kujenga mustakabali kwa siku zijazo.

Kwa mujibu wa Sheria ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania ya mwaka 2003, miongoni mwa kazi za TCRA ni kufuatilia utoaji wa huduma katika sekta inazozisimamia kwa kuzingatia kiwango cha upatikanaji wa huduma hizo, ubora na viwango vya huduma, bei ya huduma na kuhimiza ushindani na ufanisi wa kiuchumi. Katika kutelekeza majukumu yake, TCRA inawajibika kupitia na kuchambua, mara kwa mara, utoaji wa huduma katika sekta na kuchukua hatua dhidi ya chochote kinachotokea kwenye soko, kiwe chanya au hasi.

Kategori

Kategori