MECHI YA MTANI JEMBE YAINGIZA MIL 422/-

MECHI YA MTANI JEMBE YAINGIZA MIL 422/-

Mechi ya Nani Mtani Jembe kati ya Yanga na Simba iliyochezwa juzi (Desemba 21 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na Simba kuibuka na ushindi wa mabao 3-1 imeingiza sh. 422,611,000.

Mapato hayo ni kutokana na washabiki 52,589 waliokata tiketi kushuhudia mechi hiyo kwa viingilio vya sh. 5,000, sh. 7,000, sh. 10,000, sh. 15,000, sh. 20,000 na sh. 40,000. Kiingilio cha sh. 5,000 ndicho kilichovutia watazamaji wengi ambapo walikuwa 19,044.

Asilimia 18 ya Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa kutokana na mapato hayo ni sh. 64,466,084.75 wakati gharama za kuchapa tiketi ni sh. 7,488,000.

Mgawo mwingine ilikuwa kama ifuatavyo; kila klabu imepata sh. 117,470,066.61, asilimia 15 ya uwanja ni sh. 52,598,537.29, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 35,065,691.53 wakati gharama za mchezo zilikuwa sh. 28,052,553.22.

MALINZI, MKUTANO WA WAANDISHI WA HABARI

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi atakuwa na mkutano na waandishi wa habari utakaofanyika kesho (Desemba 24 mwaka huu).

Mkutano huo utafanyika saa 6 kamili mchana kwenye ukumbi wa mikutano wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).


Boniface Wambura Mgoyo
Kaimu Katibu Mkuu
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

BEI ZA UMEME JUUU...... TANESCO YAZIDI KULEMEWA NA MADENI SASA YAFIKIA BILIONI 456.8 MIZIGO WABEBESHWA WANANCHI.

Mamlaka wa udhibiti wa nishati na maji EWURA hii leo jijini Dar es salaam wametangaza kupanda kwa bei za umeme ifikapo Januari 1. 2014 kutoka asilimia 67.87 kutoka asilimia 40.29 bei inayotumika hadi hivi sasa.


 Akitangaza ongezeko la bei hizo Mkurugenzi wa udhibiti uchumi wa EWURA Bwana Felix M.Mngamlagosi amesema wamepandisha bei hizo kutokana na Tanesco kuelemewa nakuwa shirika hilo lina hali mbaya kifedha.



"EWURA imebaini kwamba hali ya kifedha ya shirika la umeme sio nzuri kwani limeendelea kupata hasara ya shilingi Bilioni 47.3 katika mwaka 2010 mpaka kufikia Bilioni 223.4 mwishoni mwa mwaka 2012, hivyo kuinusuru shirika hilo tumekubaliana kuongeza bei za umeme"amesema Felix

RIPOTI YA TOKOMEZA UJANGILI YA THIBITISHA SERIKALI KUUSIKA NA VITENDO VYA MAUAJI, UBAKAJI, UDHALILISHAJI NA UKIUKWAJI WA HAKI ZA BINADAMU

JK APEWA RUNGU KUAMUA,
PINDA NAYE MAJI YA SHINGO,
MAWAZIRI WA 4 MATUMBO JOTO BUNGE LATAKA WAVULIWE MADARAKA,WAMTAKA KAMANDA ALIYE SIMAMIA ZOEZI HILO..........


Kutoka Bungeni Dodoma




Wabunge wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania hii leo wameungana na kukemea matendo ya kikatili yaliyofanya kipindi cha zoezi la “TOKOMEZA UJANGILI ” na kumtaka Waziri mkuu Mhe. Mizengo Pinda kujiuzulu wadhifa wake kwa kushindwa kuwa simamia Mawaziri ambao zoezi hilo lilifanywa chini ya Wizara zao.


Mawaziri hao ni Mhe. Shamsi Vuai Nahodha ambaye ni Waziri wa Ulinzi, Mhe Emmanuel Nchimbi ambaye ni Waziri wa mambo ya ndani ya Nchi, Mhe. Balozi Hamis Kagasheki ambaye ni Waziri wa Maliasili na utalii na Mhe. Mathayo David Mathayo ambaye ni Waziri wa Uvuvi na Maendeleo ya Mifugo

SERIKALI YASEMA ITAHAKIKISHA FEDHA ZA MAENDELEO ZINAWAFIKIA WALENGWA

Serikali ya Tanzania inajipanga kuchukua hatua endelevu katika kuhakikisha fedha kwa ajili ya maendeleo zinazotengwa kwa kila sekta zinafikia walengwa kwa wakati.

HONGERA KENYA KWA MIAKA 50 YA UHURU

Rais Uhuru Kenyatta jana amewaongoza wananchi wa Kenya kusherehekea miaka 50 ya uhuru, na kuwataka kudumisha umoja na moyo wa uzalendo ulionyeshwa na wapigania uhuru wa Kenya, kwa kudumisha amani na mshikamano katika taifa hilo.

WANAOSEMA TUME YA UCHAGUZI SIO HURU, NI WAONGO !

Tume ya taifa ya uchaguzi nchini Tanzania imesema ina uhuru wa kutosha kuendesha chaguzi mbali mbali ikiwamo kura ya maoni ya katiba mpya, tofauti na ambavyo wadau wengi wamekuwa wakidai kuwa tume hiyo sio huru.

TANZANIA BADO INAIDAI UGANDA FIDIA YA VITA

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inategemea kulipwa na serikali ya Uganda kiasi cha dola za Marekani  milioni nane laki nane na alfu 24, ikiwa ni fedha za fidia ya vita ambayo Tanzania ilipigana nchini Uganda Miaka ya 1977/78.

WEMA ALIPA FAINI YA LAKI MOJA NA KUENDELEA KUPETA MTAANI


Ile kesi ya kumpiga na kumtukana matusi ya nguoni Meneja wa Hoteli ya Mediteranian iliyopo Kawe Beach, Dar, Godlucky Kayombo iliyokuwa ikimkabili Wema Sepetu imetolewa hukumu yake baada ya Wema kuomba iharakishwe kwakuwa alikuwa anasafari.

TANZANIA KUOMBOLEZA KIFO CHA MANDELA KWA SIKU 3

Rais wa Jamhuri Ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemtumia Salamu za rambirambi Rais Jacob Zuma wa Afrika ya Kusini na kupitia kwake, kwa mkewe Bi. Graca Machel, wanafamilia wote na wananchi wote wa Afrika ya Kusini kufuatia kifo cha Mzee Nelson Mandela kilichotokea tarehe 5 Desemba, 2013 baada ya kuugua kwa muda mrefu.
ONDOA VIKWAZO FUNGUA MILANGO YA KUJENGA JAMII JUMUISHI KWA WOTE

ONDOA VIKWAZO FUNGUA MILANGO YA KUJENGA JAMII JUMUISHI KWA WOTE


Watu wenye ulemavu wametakiwa kutokuwa wanyonge na badala yake wajitokeze na kujishugulisha na shuguli mbali mbali katika jamii

Hayo yamesemwa na Mratibu wa kitengo cha walemavu kutoka hosptali ya CCBRT bwana Fredrick Msigana wakati akiongea na Blog hii mwishoni mwa wiki jijini Dar es salaam.

Bwana Fredrick amesema walemavu wamekuwa wanyonge kila mara hivyo wanakosa fursa zingine ambazo wangeweza kujitokeza kuzifanyia kazi na kusema kuwa siku ya walemavu duniani itakuwa fursa kubwa kwao

JK: VIJIJI 155 KUNUFAIKA NA MRADI WA UMEME, VINGINE 1449 KUNUFAIKA NA MAJI HUKO SHIMIYU:

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amesema kuwa Serikali yake itaongeza kwa kiasi kikubwa kasi ya kusambaza huduma za umeme na maji vijiji kwa nia ya kuboresha maisha ya wananchi wake


Rais Kikwete ameyasema hayo wakati akizindua miradi ya maendeleo hii leo, katika ziara yake ya mara ya kwanza katika mkoa mpya wa Shimiyu ambapo mamia ya wananchi walihudhuria uzinduzi wa miradi hiyo

Rais Kikwete ameanza ziara hiyo kwa kuweka jiwe la msingi kwenye ujenzi wa Barabara ya Bariadi-Lamadi kwa kiwango cha lami katika sherehe iliyofanyika katika eneo la Old Maswa katika Wilaya hiyo.

DKT. GHARIB BILAL “UKIWA NA VIRUSI VYA UKIMWI USIWAAMBUKIZE WENGINE”

 
Wananchi wametakiwa kutowaa mbukiza wengine virusi vya ukimwi, Wajikinga na maambukizi mapya pamoja na kuwa na uelewa wa ugonjwa wa ukimwi ili kupunguza madhara ya gonjwa hilo hapa nchini



Hayo yamesemwa na Makamu wa Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Dkt Mohamed Gharib Bilal alipokuwa akivishwa Beji ya kupiga vita dhidi ya Virusi vya ukimwi katika wiki hii ya kuelekea maadhimisho ya siku ya Ukimwi Duniani na Viongozi wa Umoja wa vijana CCM jijini Dar es salaam.

AIBU: JIBABA LAFUMWA NA DENTI WA SHULE YA MSINGI

MZEE mmoja kigogo wa biashara ya kuuza mbao jijini Dar es Salaam, hivi karibuni alinaswa kitandani ndani ya chumba akiwa na mrembo aliyedaiwa ni mwanafunzi wa shule moja ya msingi Tegeta Wazo, Dar.

P- SQUARE WAKANUSHA KUMFAHAMU DIAMOND

Mwanamuziki wa P square, Peter Okoye ameoneshwa kushangazwa na taarifa kwamba mwanamuziki wa bongo fleva Naseeb Abdul alihudhuria harusi yake hivi karibuni nchini Nigeria na kuhudhuriwa na mastaa mbali mbali akiwenmo msukumba gozi wa Totenham Hotspurs Adebayor.

P-SQUARE WAAHIDI SHOO YA NGUVU BONGO, NI MWENDO WA PESONALITY

Kundi la P-SQUARE lililotua jana nchini Tanzania toka Nigeria kwa ajili ya tamasha kubwa litakalofanyika siku ya kesho pale Leaders club wameahidi kutoa burudani yenye kiwango cha juu kwa watanzania wote watakaohudhuria.

Zimbabwe kutua mchana leo kuikabili Taifa Stars

Kikosi cha Zimbabwe kinawasili leo mchana (Novemba 18 mwaka huu) kuikabili Taifa Stars katika mechi ya Kalenda ya Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA)- FIFA Date itakayofanyika kesho (Novemba 19 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Diamond ahudhuria harusi ya Peter wa P-Square

My number one singer Diamond Platinumz ambaye yupo Nigeria kwa sasa akiwa anafanya remix ya My Number One akiwa anashirikiana na Davido. Akiwa Nchini Nigeria Diamond alipata mualiko wa kuhudhuria harusi ya Peter wa P Square.

Pichani ni Diamond Platnumz msanii kutoka bongo akiwa na bwana harusi Peter wa Psquare pale walipokutana huko Lagos Nigeria kwenye harusi ya Peter.

Pinda apewa siku 7 kutoa ripoti ya Elimu

Waziri mkuu wa Tanzania Mhe. Mizengo Pinda amepewa siku 7 ili kutoa hadharani ripoti ya tume ya aliyounda kuchunguza matokeo ya kidato cha nne mwaka 2012 ambapo takribani asilimia 60 ya watahiniwa walifeli mitihani hiyo

Tanzania kukaa giza kwa siku 10 bila umeme

Shirika la umeme nchini Tanzania Tanesco limetangaza kuwepo kwa umeme wa mgao kuanzia tarehe16 mpaka 26 mwezi huu kutokana na upungufu wa gesi katika kisiwa cha songosongo kilichopo wilayani Kilwa kuwa na matengenezo ya kiufundi

Poulsen aunda kikosi kuikabili Harambee Stars


Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Kim Poulsen ameunda kikosi cha wachezaji 32 kwa ajili ya mechi ya kirafiki ya kimataifa dhidi ya Kenya (Harambee Stars) itakayochezwa Jumanne, Novemba 19 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
TANZANIA KUCHANGIA ASKARI KATIKA KIKOSI CHA AFRIKA

TANZANIA KUCHANGIA ASKARI KATIKA KIKOSI CHA AFRIKA

Tanzania ni miongoni mwa nchi tano za Afrika ambazo zimejitolea kutoa askari wa kuunda Kikosi cha Kukabiliana na Migogoro ya Kijeshi Barani Afrika cha African Capacity for Immediate Response to Crises (ACIRC) kitakachoundwa kwa mujibu wa uamuzi wa Wakuu wa Nchi Wanachama wa Umoja wa Afrika (AU).
 
Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari hapa nchini na ikulu ya Tanzania inasema Tanzania itatoa kikosi kimoja (Battalion Group) na nchi nyingine ambazo zimekubali kuchangia askari ama polisi 



Katika Kikosi hicho ni Afrika Kusini, Uganda, Algeria na Chad. Nchi hizo zilijitokeza kushiriki katika Kikosi hicho wakati wa Mkutano wa Wakuu wa Majeshi wa nchi hizo huko Pretoria, Afrika Kusini, 

Mkutano ambao maamuzi yake yameidhinishwa na kukubaliwa na wakuu wa nchi akiwamo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete. 
 
ACIRC kitakuwa kikosi cha muda wakati Afrika inaendelea na maandalizi yake ya kuunda Jeshi la Kudumu la Afrika (Africa Standby Force) na Lenye Uwezo wa Kukabiliana na Migogoro Haraka na Popote barani humu (Rapid Deployment Force).

Jeshi hili litakuwa ni jeshi lenye uwezo wa kuingia nchi yoyote, chini ya AU, na hivyo wakati mwingine litatumika kutuliza migogoro katika nchi yoyote ya Afrika hata kama nchi husika haijaomba msaada wa jeshi hilo.

Jeshi hilo litakalofanya kazi yake chini ya mfumo wa Amani na Usalama katika Afrika – African Peace and Security Architecture (APSA) litaiwezesha AU kuwa na jeshi la askari na polisi wenye uwezo na nguvu kukabiliana na mizozo ya kijeshi barani humo na kuwa vifaa vyake vitatolewa nchi wanachama wa AU ambao watakuwa tayari kushiriki katika mpango huo.
KIASI BILLIONI 2.6 CHATOLEWA KUSAIDIA WASAFIRISHAJI UKANDA WA ASFIKA MASHARIKI, WATANZANIA WATAKIWA KUCHANGAMKIA FURSA HIYO

KIASI BILLIONI 2.6 CHATOLEWA KUSAIDIA WASAFIRISHAJI UKANDA WA ASFIKA MASHARIKI, WATANZANIA WATAKIWA KUCHANGAMKIA FURSA HIYO





Watanzania wanao jihusisha na biashara ya usafirishaji wametakiwa kuchangamkia kiasi cha Pound Milioni 100 kilichotolewa na serikali ya Uingereza ambayo ni sawa na shilingi Bilioni 2.6 za kitanzania ili kuwasaidia katika kupata mitaji na kuendesha biashara zao


Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Wizara ya Uchukuzi Dr. Charles Tizeba wakati wa uzinduzi wa mfuko wa kusaidia wachukuzi kupunguza garama za kusafirisha mizigo katika ukanda wa afrika mashariki mkutano uliohudhuriwa na Balozi wa Uingereza, na ziongozi wa jumuhiya ya Afrika mashariki

ASHANTI UTD, SIMBA UWANJANI VPL  HUKU TFF  IKITAKA  ORODHA YA WALIO SAMEHEWA

ASHANTI UTD, SIMBA UWANJANI VPL HUKU TFF IKITAKA ORODHA YA WALIO SAMEHEWA



Mechi za kukamilisha mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) zinaanza kesho (Novemba 6 mwaka huu) ambapo Ashanti United itakuwa mwenyeji wa Simba kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.  

Viingilio katika mechi hiyo itakayochezwa kuanzia saa 10 kamili chini ya mwamuzi Andrew Shamba kutoka Pwani ni sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000. Waamuzi wasaidizi ni Abdallah Mkomwa na Rashid Abdallah wote kutoka Pwani wakati mezani atakuwa Hamisi Chang’walu.  

Mechi nyingine za kesho ni JKT Ruvu Stars na Coastal Union (Uwanja wa Chamazi), Kagera Sugar na Mgambo Shooting (Uwanja wa Kaitaba, Bukoba) na Ruvu Shooting na Mtibwa Sugar (Uwanja wa Manungu, Morogoro).

SHULE NA VYUO KUFUNGWA HUADHIRI UKUSANYAJI WA DAMU SALAMA

SHULE NA VYUO KUFUNGWA HUADHIRI UKUSANYAJI WA DAMU SALAMA



Watanzania wameombwa kuendelea kuchangia damu kwa hiari hasa katika kipindi hichi cha mwezi Nov mpaja January kutokana na shule na vyuo vingi kufungwa kwani wachangiaji wengi wa damu ni wanafunzi ambao watakuwa likizo kwa miezi hiyo.


Wanafunzi wa vyuoni pamoja na wale wa shule za sekondari ndio wamekuwa wakijitolea kwa kiasi kikubwa katika upatikanaji wa damu salama hivyo muda wa likizo idadi ya upatikanaji wa damu salama hupungua.

MCHAKATO WA KATIBA MPYA: AZAKI YALIA NA USHIRIKI WA WANANCHI BUNGE LA KATIBA, WAOMBA KURA YA MAONI IFANYIKE KATIKATI YA WIKI

MCHAKATO WA KATIBA MPYA: AZAKI YALIA NA USHIRIKI WA WANANCHI BUNGE LA KATIBA, WAOMBA KURA YA MAONI IFANYIKE KATIKATI YA WIKI



Wakati rasimu ya pili ya katiba mpya ikisubiriwa kwa hamu na wananchi pamoja na wadau mbalimbali ili bunge la katiba liweze kuundwa kwa ajili ya kujadili rasimu ya katiba hiyo,




 Asasi za kiraia zaidi ya 37 zimeendelea kulia na idadi ya ushiriki wa wananchi katika mchakato huo kwa kuhofia idadi ya Wabunge ambao watahitaji kuunda Bunge la katiba.


Akitoa maazimio mbele ya wanahabari hii leo jijini Dar es salaam, juu ya Sheria ya marekebisho ya katiba sura namba 83, Bunge maalum la katiba, kura ya maamuzi au maoni. Tume ya marekebisho ya katiba pamoja na maudhui ya katiba hiyo.

Kategori

Kategori