MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2012 YATOKA, WASICHANA WABURUZWA, MATUSI NA UDANGANYIFU VYA JIRUDIA TENA



Matokeo ya kidato cha nne 20012 yametoka hii leo, huku wasichana wakiwa wameburuzwa sana na wavulana kwa kiwango cha ufaulu. Matokeo hayo yametangazwa katika wizara ya elimu na mafunzo ya ufundi jijini Dar es salaam na waziri wa wizara hiyo Mhe. Shukuru Kawambwa

Octoba mwaka jana, Jumla ya watahiniwa Laki 126, 847 elfu walifanya mtihani huo, waliofaulu ni wanafunzi 397,136 huku wasichana wakiwa ni Elfu 46 na161 na wavulana niElfu 80 na 686. idadi inayofanya wavulana kuwajuu zaidi ya ile ya wasichana

Waziri amesema, Jumla ya watahiniwa Elfu 23, mia 520 wamefaulu katika daraja la I-III ambapo katiyao wasichana ni Elfu 7,178 na wavulana ni Elfu 16,342 ambapo wasichana wameburuzwa kawa kiasi kikubwa pia

Shule 10 zilizofanya vizuri ni, St. Francis Girls iliyopo Mbeya, Marian Boys iliyopo Pwani, Feza Boys iliyopo Dar, Marian Girls iliyopo Pwani, Rosmini iliyopo Tanga, Canosa iliyopo Dar, Jude Moshono iliyopo Arusha, St.Marys mazinde juu iliyopo Tanga, Anwarite Girls iliyopo Kilimanjaro na Kifungilo Girls iliyopo Tanga

Shule 10 zilizofanya vibaya ni Mibuyuni – Lindi, Ndame – Unguja, Mamndimkongo – Pwani, Chitekete – Mtwara, Maendeleo – Dar es salaam, Kwamndolwa – Tanga, Ungulu – Morogoro, Kikale – Pwani, Nkumba – Tanga na Tongoni pia kutoka Tanga

Wanafunzi 24, wamefutiwa mitihani yao kwa sababu ya kuandika matusi katika script zao, “ Waziri amesema kutokana na kosa hilo baraza la mitihani limefuta matokeo yao yote kwa mujibu wa kifungu cha 6 (2)a cha kanuni za mitihani”.

Akitoa tadhmini ya ufaulu wa mitihani hiyo, Waziri amesema shule zilizo fanya vibaya zaidi nizile za vijini ambazo hazina kabisa walimi, miundombinu ni mibovu, hakuna maabara kwaajili ya masomo ya sayansi, kuna ubungufu mkubwa wavitabu na changamoto mbalimbali

“ Shule hizi zilizofanya vibaya zinachanga moto nyingi kama nilivyo taja na Serikali inajitahidi kuzuia changamoto hizo ilikukabiliana nayo, kwa kuajiri walimu wapya Elfu 13,246 ” Alisema Waziri

MWANAFUNZI BORA HAJAWEKWA HADHARANI

Katika hali ya kushangaza Wizara haikuweza kumuweka hadharani mwanafunzi bora wa mwaka 2012 wa kidato cha nne kama inavyo fanya miaka yote, akijibu swali lililo ulizwa na mwandishi wa habari katika mkutano huo waziri amesema

“ Sikuweza kuandaa nimwanafunzi yupi ameshika nafasi ya kwanza kutokana na wengi kugongana kwa alama, lakini niombe samahani kwa hilo na mtajulishwa baadae” Alisema waziri

Aidha aikutolewa tadhmini ya ufaulu kwa mwaka 2011 na hii ya 20012 kwa kidato cha nne ilikujua kama kiwango kimeshuka au laah. TAKWIMU AMBAZO KILA MWAKA HUTOLEWA


EmoticonEmoticon