WIZARA YA ELIMU IAMISHIWE OFISI YA RAISI, WAZIRI WA ELIMU NAYE AWAJIBIKE KISA MATOKEO KIDATO CHA NNE 2012: ZITTO ANENA


> SIFURI ZA MTISHA ZITTO
> ASISITIZA WIZARA YA ELIMU IAMISHIWE OFISI YA RAISI
> AMTAKA WAZIRI AWAJIBISHWE
> AHOJI JUU YA ELIMU YA VYUO VYA UFUNDI, AKITABIRI TAIFA LA MAMBUMBUMBU
> ASISITIZA BILA ELIMU NIBURE

Taarifa ambayo Mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe ameiandika kwenye ukurasa wake wamitandao ya kijamii,kuusiana na matokeo ya kidato cha nne 2012, ambapo mbunge huyo ameitaka wizara ya Elimu kuwajibishwa na kuiamisha kwenda ofisi ya raisi

Tarifa ya Zitto inasema, Matokeo ya Kidato cha Nne ya namna hii (zaidi ya nusu ya wahitimu kupata sifuri) na takribani asilimia 90 kufeli kwa kupata daraja la nne na daraja la sifuri kwa mwaka wa tatu

Zitto amesema kuwa,Waziri lazima awajibike na Naibu wake na Katibu Mkuu na Kamishna, Najua kuwa haina uhusiano wa moja kwa moja maana matatizo ya elimu ni makubwa sana nchini. Lakini ni lazima kitu fulani kitokee ili kufanya mabadiliko. amesema zitto

Aidha amesema, Tumwambie Rais aichukue Wizara ya Elimu, yaani Waziri wa Elimu awe yeye (kuwe na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Elimu). Tumwambie matokeo yakibaki hivi mwakani na yeye atatoka. kwani kwa kutofanya hivyo mwakani pia haya yatajirudia.

Mhe. Zitto ameendelea kusema, Mwaka jana tulisema mpango wa kujenga vyuo vya ufundi kila Halmashauri ya Wilaya uanze mara moja. Katika Bajeti Kivuli mwaka 2011 tulipiga hesabu kwamba tunahitaji tshs 720 bilioni katika kipindi cha miaka 5 ijayo kujenga vyuo vya ufundi vya VETA kila Wilaya. 

Aliongeza kuwa, Tukawaambia badala ya kukopa kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii kulipana posho ni vema tukope kuwekeza kwenye elimu maana Elimu ni Hifadhi ya Jamii. Elimu yetu ya sasa inazalisha matabaka kwenye jamii na ni hatari sana kwa uhai wa Taifa.

Aidha, Tunaweza kujidai kujenga madaraja na miji mipya. Tunaweza kujidai kujenga mabomba ya gesi na kusambaza umeme kila kijiji mpaka kwenye vyoo. Kama hakuna Elimu haya yote ni bure kabisa. Hata kukosa uvumilivu wa kiimani sasa hali itakuwa mbaya zaidi unapokuwa na Taifa la mambumbumbu. Waziri Shukuru Kawambwa na wenzake watoke. Watoke SASAalimalizia Zitto 
 
UBORA NA UFAULU KWA DARAJA KIDATO CHA NNE 2012

DARAJA
(division)
IDADI YA WAVULANA IDADI YA WASICHANA JUMLA
I 1073 568 1641
II 4456 1997 6453
III 10813 4613 15426
IV 64344 38983 103327
0 120664 120239 24090

Idadi ya matokeo kama ilivyo kwenye jedwari nikwamba wanafunzi waliopata Division I ni Elfu 1641 katika taifa zima, waliopata Division II ni Elfu 6453, Division III ni Elfu15,426, Division IV ni Laki103,327 huku Division 0 ni Laki 240,903 matokeo ya kidato cha nne 2012


EmoticonEmoticon