PISTORIUS AMWAGA MACHOZI MAHAKAMANI, AKISOMEWA KESI YA MAUAJI


Akisomewa mashitaka hii leo mahakani. Afrika Kusini
Mwanariadha mlemavu wa Afrika kusini Oscar Pistorius leo amemwaga chozi wakati akisomewa mashtaka ya mauaji ya mpenzi wake katika mahakama ya jijini Pretoria. Tukio alilofanya siku ya valentines day

Star huyo wa mashindano ya Olympic ya walemavu mwenye umri wa miaka 26 alishika kichwa kwa masikitiko mara baada ya shitaka lake la kwanza kutajwa na Hakimu wa mahakama hiyo 
Akiwa uwanjani akijiandaa kukimbia (Marathon 2012)
Hakutakiwa kujibu chochote katika kesi hiyo ingawa ndugu, jamaa na uongozi wake unapinga kwa nguvu zote tuhuma zote zinazoelekezwa kwake kwamba alimuua kwa makusudi mpenzi wake Reeva Steenkamp, mwenye umri wa miaka 29, alfajiri ya kuamkia siku ya Valentine

Waendesha mashtaka wa kesi hiyo wameieleza mahakama kuwa yalikuwa ni mauaji ya kukusudia na kupanga yanayostahili adhabu ya kifungo cha maisha

 
Aliposikia hivyo, Oscar alishtuka kwa hisia kali sana za huzuni na uchungu lakini hatahivyo baba yake mzazi pamoja na ndugu zake waliokuwepo mahakamani hapo walimfariji na kumtia moyo

 
Oscar Pretorius akiwa na mpenzi wake huyo siku zanyuma

Minong'ono ilisikika mahakamani hapo baada ya bastola anayotuhumiwa kuitumia katika mauaji hayo kuletwa mahakani hapo ikiwa ndani ya mfuko wa Plastik ikiwa imebebwa na polisi

Vyombo mbalimbali vya habari nchini Afrika K usini zimesema kuwa asubuhi ya siku yatukio hilo, walimkuta Oscar akiwa amekaa pembeni ya mwili wa Steenkkamp akiwa amekwisha kufa


EmoticonEmoticon