HAKUNA MGAO WA UMEME TANESCO WAFUNGUKA, HABARI ZA KUZIMWA MITAMBO YA SONGAS, BWAWA LA MTERA YAKANUSHWA,



Shirika la umeme Tanesco limewatoa hofu wanachi kwa kukanusha juu ya kuzimwa kwa mitambo ya Songas pamoja na kukauka kwa bwala la Mtera, na kusisitiza kuwa hakuna mgao wa umeme kwa sasa, hayo yamesemwa na Bi Badra Masoud ambaye ni msemaji wa TANESCO

Pia Shirika hilo limewaomba radhi Wananchi wanaofikwa na usumbufu pindi umeme unapo katika kwani shirika hilo linadhamira ya dhati ya kutatua matatizo ya umeme nchini. Alisema Badra

“Mitambo ya Songas haita zimwa, wala Bwawa la Mtera halija kauka kiasi cha kuzima uzalishaji wa umeme katika bwawa hilo japokuwa kiwango cha uzalishaji kimepungua kutoka Megawati 80 mpaka Megawati 40 lakini aiwezi kufanya tukazima mitambo hiyo, tutatumia kiwango cha umeme kinacho patikana na sio kuzima mitambo hiyo” Alisema Bi Badra

Akifafanua zaidi juu ya swala la Kampuni ya Songas kuzima mitambo yake Bi Bibadra amesema, Kampuni hiyo tayari imepewa kiwango cha fedha ya Deni wanalo dai japo kuwa hawajamali kulipa deni hilo. Hatahivyo Bi Badra alisikitishwa na kitendo cha kampuni ya Songasi kusema kwenye vyombo vya habari kuwa inaidai Tanesco na kuwa itazima mitambo yao ilhali njia za mazungumzo kati yao inaendelea

“Sivyema kwa Songas kulalamika kwenye vyombo vya habari, kama Tanesco wameshindwa kuelewana na sisi yupo baba yetu mama yetu Wizara ya Nishati na Madini waende kule na kulalamika na madai yao yatasikilizwa lakini tayari wamelipwa kiasi fulani cha pesa” ...hakuweka wazi kiasi walicholipa.

AIDHA Tatizo lililopo hizi sasa ni marekebisho ya miundombinu ambayo yanaendelea kote nchini kwani kwamuda wa miaka 10 shirika hilo halikuwekeza kwenye miundombinu, hali inayopelekea kuwepo kwa uchakavu wa Nguzo, Nyaya na miundombinu muhimu. Alisema Bi Badra

“Hivi sasa marekebisho ya miundombinu yanaendelea maeneo mbalimbali hali inayopelekea kukatika kwa umeme, marekebisho yatachukua muda lakini tunaomba watanzania wawe wavumilivu' hali hii itaisha, kikubwa nikuweka sawa miundombinu yetu” Alisema

Sabubu ambazo Bi Badra aliziita kuwa ni UN PLANED SHUT DOWN, nimiongoni mwa matatizo yanayopelekea umeme kukatika baadhi ya maeneo akitolea mfano, kuibwa kwa nyaya za umeme, kukatika kwa nguzo za umeme, wizi wa mafuta ya transfoma na mengine mengi kama mvua kali au upepo mkali nimiongoni mwa mambo yanayopelekea umeme kukatika.

Shirka la hilo linasikitishwa na kukatoka kwa umeme hata kwa sekunde moja kwani hali iyo inapotokea uinyima mapato shirika hilo na kuieleza jamii kuwa inania ya dhati ya kuboresha matatizo yaliyopo hivi sasa, ilikuzuia matatizo ya kukatika kwa umeme

Kwa zaidi ya mwezi sasa Umeme umekuwa ukikatika katika maeneo mengi ya Jiji la Dar es Salaam, na maeneo mengine hali iliyopelekea wananchi kuhoji endapo kuna mgao wa umeme lakini Tanesco wamekanusha kuwepo kwa Mgao licha ya umeme kukatwa mara kwa mara


EmoticonEmoticon