WANAWAKE ELFU 4300 HUFARIKI KILA MWAKA KUTOKANA NA SARATANI YA KIZAZI



Miongoni mwa wanawake Elfu 6200 ambao hugundulika kuwa na Saratani, katiyao wanawake Elfu 4300 ufariki kila mwaka kwa ugonjwa huo. Wengi wawana wake hao niwenye umri kati ya miaka 15 na 44 ambao usumbuliwa na Saratani shingo ya kizazi

Akiongea le jijini Dar es salaam katika uzinduzi wa mpango wa pamoja wenye lengo la kudhibiti tatizo hilo, Waziri wa Afya na Ustawi wa jamii Mhe. Dkt Hussein Mwinyi amesema, Serikali pamoja na wadau wenye nia ya kusaidia taifa watashirikiana juu ya ugonjwa huo

"Niwanawake Elfu 4300 ndio wanao fariki kutokana na saratani ya shingo ya kizazi kila mwaka, miongoni mwa wale Elfu 6200 ambao hugundulika kuwa na ugonjwa huo hapa nchini" Alisema Dkt Mwinyi 

Aidha Waziri aliwataja Wadau hao kuwa ni Chama cha Wazazi na Malezi (UMATI), Marie stopes international pamoja na PSI, Ambao kwa pamoja wametangaza nia yakuungana na serikali katika kudhibiti tatizo la kansa ya shingo ya kizazi

Hatahivyo, Waziri amewataka wanawake na watu wengine kwa ujumla kujijengea tabia ya kwenda kucheki Afya yao ilitatizo liweke kudhibitiwa mapema

Kwa mujibu wa tafiti za Afya Duniani, hivi sasa ugonjwa wa Saratani (Cancer) ndio ugonjwa unaoongoza kwa kuuwa watu wengi zaidi ikifuatiwa na Maleria na Ukimwi


EmoticonEmoticon