NINAHAKIKA HUYU SIMFANYAKAZI WA TANESCO IRINGA


Kwamujibu wa mtandao wa Jamii Forums, Fundi wa Shirika la Umeme Tanesco mkoani Iringa, Selemani Mbuma akiwa amenaswa na umeme baada ya wenzake kuwasha umeme kimakosa wakati akiendelea na matengenezo katika eneo la Mlandege mkoani humo.

Picha hii inamengi ya kuzungumzia, kama kweli ni fundi umeme basi akujipanga kwani huwezi kupanda huko juu na anajua kiasi cha umeme kinachopita hapo (Volt), bila kuweka mazingira ya thahadhari yoyote

Hajavaa kitu chochote cha kufunika umeme na miguu yake kama anavyoonekana pichani, kuanzia miguuni mikononi mpaka kichwani..... hatakama tutamtafuta mkosaji binafsi sijui ninai kwani yeye tu hakuonyesha nia ya kujisaidia

Hii iliwahi kutokea hapa Dar maeneo ya Jogoo kufuatilia sana kumbe alikuwa ni kibarua sasa TANESCO muwafundishe vibarua wenu kabla ya kuwapa ajira ninauhakika huyu simfanya kazi wa Tanesco na alikuwa kibarua tu.....

Kama nimfanya kazi kweli nina mashaka na uongozi wake pamoja na watu alioongozana nao mpaka anapanda huko juu bila hata Element,

Nakama ilikuwa inajulikana kuwa kunawatu wanafanya matengenezo haja ya kuwasha umeme ilitokana na nini mpaka umauti ukamkumba Selemani Mbuma, Tanesco wafundisheni vibarua na kuweni na mawasiliano nao ilikuepuka vifo vinavyo epukika


EmoticonEmoticon