TCRA: WALIOKIUKA MAADILI YA HABARI WAFUNGIWA


Mamlaka ya mawasiliano Tanzania (TCRA) imevifungia Radio mbili pamoja na kipengele kimoja katika kipindi cha radioni kwa kile walichodai ni ukiukwaji wa maadili ya habari

Akizungumza na waandishi wa habari hii leo katika ukumbi wa habari maelezo jijini dar es salaa, Makamu Mwenyekiti wa tume ya maudhui kutoka TCRA Dr. Wolter Bugoya ametangaza maamuzi hayo huku akisisitiza watangazaji na waandishi wa habari kufuata maadili
Tumefungia matangazo kwa muda wa miezi sita kwa vituo viwili vya Radio, kwakukiuka maadili ua utangazaji, na kipengele kimoja tumeamuru kifutwe kabisa kutokana na kuchochea mambo mabaya katika jamii” alisema
Vituo hivyo ni pamoja na KWA NEEMA FM ambayo ipo mkoani Mwanza, ambayo imefungiwa kwa kuendesha mjadala uliokuwa ukihusisha watu wa dini gani wenye haki ya kuchinja wanyama kati ya waislamu na wakristo hali iliyo sababisha mgongano wa kiimani wa dini mpaka kupelekea mauaji na mabishano. Alisema
RADIO IMANI FM ya mkoani Morogoro, imefungiwa kwa kosa la kupnga zoezi la SENSA mwaka jana na kuwashawishi waumini wa dini ya kiislamu wasijiandikishe kwenye zoezi hilo. Alisema Dr.Buya
Aidha Kipindi cha Power Breakfast kinachoruka kila siku asubuhi katika Radio CLODS FM, kimefungiwa kabisa kipengele kinachoitwa JICHO LA NG'OMBE ambacho kinaruka kwenye kipindi hicho, ambapo licha ya kupigwa marufuku ila kimefungiwa kabisa.
Tumefungia kipengele cha jicho la ngo'mbe na kwamba kisianzishwe kingine chenye maudhuhi hayo wala kurusha kipegele kama hicho tena, kama Clouds Radio itarudia basi hatua zingine zitachukuliwa “ Alisema Dr. Buya
Hatahivyo Clouds Radio imetakiwa kulipa kiasi cha Shilingi Milioni 5 za kitanzania kama faini juu ya kile walicho dai ni uchochezi kwa mambo ya kishoga, kulingana na mada waliojadili juu ya Mtoa sala wa Nchini Marekani ambaye aliwaombea mashoga kipindi cha uchaguzi wa marekani” Alisema Dr. Buya
Mamlaka ya mawasiliano Tanzania, TCRA kupitia kitengo cha maudhui kimetoa onyo kwa waendesha vipindi kuwadhibiti wasikilizaji wao hasa wanapotoa maoni kwani kutofanya hivyo kutawapa mwanya kutoa maoni yaliyona uchochezi kwa jamii


EmoticonEmoticon