BUNGE LAVURUGIKA NA KUAHIRISHWA , KAULI YA WAZIRI MKUU MHE. PINDA YASUBIRIWA KWA HAMU



Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo asubuhi amelazimika kusitisha shughuli za bunge baada ya wabunge kutaka serikali kuahirisha mchakato wa kura ya maoni pamoja na kutoa taarifa ya uandikishwaji wa wapigakura kwa kutumia mfumo wa kielektroniki wa BVR.




Wakichangia hoja bungeni Mbunge wa Kisarawe Mh. Suleiman Jaffo na Mbunge wa Ubungo Mh. John mnyika wametaka suala hilo lijadiliwe kama dharura na kutolewa majibu na serikali kuhusu hatama ya mchakato huo.

Taharuki ilizuka baada ya Spika wa Bunge hilo Mhe. Makinda kutaka kuzitupilia mbali hoja hizo. Wabunge walianza kupiga kelele kutaka majibu ya serikali papo hapo na ndipo Spika wa bunge alilazimika kuhairisha kikao hicho mpaka jioni ambapo leo ni kikao cha mwisho cha bunge hilo.

Mnyika “ Nimesimama kupata Idhini kwa mujibu wa kanuni kuomba shuguli za mbunge zisitishwe na badala yake tujadili zoezi la uandikishwaji kwani mpaka sasa zoezi halijakamalika hata kwa mkoa mmoja, hivyo Waziri mkuu kwakuwa yupo hapa Bungeni atupe majibu nini kinaendelea” Amesema Mnyika

Spika “Hoja hii na ile ya kwanza zinafanana, majibu mtajibiwa baadae katika kikao cha jioni” Alisema spika. Aidha wabunge wa Upinzani walionesha nia ya kutaka kujua hivyo kupiga kelele kwakusema “Tuna taka Majibu” hali iliyopelekea spika wa bunge kuahirisha Bunge hadi jioni.
MABADILIKO YA MAKAMANDA WA POLISI WA MIKOA

MABADILIKO YA MAKAMANDA WA POLISI WA MIKOA

TAARIFA YA JESHI LA POLISI KWA VYOMBO VYA HABARI



Inspekta Jenerali wa Polisi IGP Ernest Mangu amefanya mabadiliko kwa baadhi ya makamanda wa polisi wa mikoa.

Miongoni mwa makamanda wa mikoa waliofanyiwa mabadiliko ni pamoja na aliyekuwa kamanda wa Mkoa wa Simiyu, Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Charles Mkumbo anakwenda kuwa kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza na nafasi yake kuchukuliwa na aliyekuwa afisa mnadhimu mkoa wa Manyara Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Gemini Mushi. Aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Valentino Mlowola anakwenda kuwa Kaimu Kamishna wa Intelijensia makao makuu.

Aliyekuwa kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Maria Nzuki amehamishwa makao makuu kuwa mkuu wa polisi jamii na nafasi yake kuchukuliwa na aliyekuwa kamanda wa kikosi cha ufundi Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Lucas Mkondya.

Wengine ni aliyekuwa Kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Godfrey Kamwela amehamishiwa Polisi Makao Makuu na nafasi yake kuchukuliwa na aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Njombe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Fulgence Ngonjani.

Aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Ulrich Matei amehamishiwa Kanda Maalum ya Dar es Salaam kuwa mkuu wa utawala na nafasi yake kuchukuliwa na aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kigoma Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Jafary Mohamed.

Kategori

Kategori