WAJUMBE WA HALMASHAURI KUU CCM TAIFA WAPATIKANA




Chama cha Mapinduzi kimepata wajumbe 14 wa kamati kuu ya Halmashauri kuu ya CCM taifa baada ya kikao cha siku mbili kilichoendeshwa huko mkoani Dodoma

Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya Habari na Katibu wa halmashauri kuu ya taifa itikadi na uenezi Bwana Nape Nnauye, anasema halmashauri kuu ya chama hicho kimeridhia na uteuzi na kufanya uchaguzi wa wajumbe hao 14 wakamati kuu

Aidha waliochaguliwa na kuibuka kidedea kwa Tanzania Bara ni Ndugu Pindi Chana, Adam Kimbisa, William Lukuvi, Dr. Emmanuel Nchimbi, Jerry Slaa, Stephen Wasira na mama Anna Tibaijuka

Kwa upande wa Tanzania Visiwani – Zanzibar, walioibuka kidedea ni Ndugu Shamsi Vuai Nahodha, Hussein Mwinyi, Prof. Makame Mbarawa, Dr Salim Ahmed Salim, Maua Dftari, Samia Suluhu na mama Hadija H Aboud.

Hatahivyo Halmashauri kuu ya Taifa ya CCM imeridhia uteuzi wa Dr. Salim Ahmed kuwa mjumbe wa Halmashauri Kuu kupitia nafasi 10 zauteuzi wa mwenyekiti wa CCM


EmoticonEmoticon