SIASA YA MALIZA UZALENDO KWA VIONGOZI, KUKATALIWA HOJA YA ELIMU BUNGENI

Naibu Spika Job Ndugai
NAIBU Spika Job Ndugai leo amekataa waziwazi kujadiliwa kwa hoja Binafsi iliyowasilishwa na Mhe. James Mbatia ambaye ni Mwenyekiti wa chama cha NCCR Mageuzi, hoja iliyowasilishwa ilikujadili udhaifu uliopo katika sekta ya Elimu nchini, 



Kitukilicho pelekea Wabunge wa upinzani kususia kikao cha Bunge na kutoka nje ya Bunge

“ Kanuni haijulikani, sikunyingine jipange vizuri zaidi” Alisema Job Ndungai na kuruhusu hoja nyingine iwasilishwe huku ya Mbatia ikitupiliwa Mbali

Job Ndugai alisikika mara kadhaa akimtaka James Mbatia asiingilie mamlaka yake pale alipokuwa akinukuu baadhi ya vipengele vya kanuni za Bunge ilikusisitiza hoja yake kueleweka mbele ya Bunge tukufu

“Hapo sasa unangilia mamlaka yangu, unavaa kiti changu kitu ambacho hakiruhusiwi kisheria” Alisema naibu spika huku mabishano yakiendelea katiyake na Mhe. mbatia

Hoja ya James Mbatia, ambayo ilikuwa na Vipengele vitatu ikiwemo ya Kutaka kujua juu ya Marekebisho ya mitaala ya elimu kwa shule za Sejkondari na Msingi, mbili Mutasari wa Vitabu vya Shule ya Msingi na vya Sekondari... pamoja na kutokuwepo kwa mitaala ya Elimu ya elimu

Mwenyekiti wa chama cha NCCR Mageuzi/ Mbunge wa kuteuliwa

“ Tuweni na Huruma, Imani na Busara na ungwana utumike katika hili, swala la heli ninalo ongelea hapa sio shule ambazo watoto wetu wanasomea ni zawatanzania wengine, na ninaongea “ Above Political Level” Alisema Mbatia kwa uchungu huku akimwambia spika kuwa hatahukumiwa

Kilio kingine cha Mhe. Mbatia ni kutowasilishwa kwa Mitaala mpaka sasa kwa wabunge huku serikali ilitoa ahadi kupitia Waziri shukuru Kawambwa mwaka jana kuwa angewasilisha mitaala hiyo ilikulidhibitishia Bunge kuwa linalopigiwa kelele sio kweli

“ Sitoendelea kujadili hoja yangu mpaka mitaala ya Elimu iwasilishwe Bungeni, ilikudhibitisha uongo ambao nimeuweka katika hoja yangu” Alisema Mbatia na kukaa chini

Baada ya halihiyo kuwepo ndipo wabunge wa upande wa Upinzani akiwemo James Mbatia waliondoka Bungeni mmoja mmoja na kuacha mjadala ukiendelea Bungeni hapo

Hali hiyo ilithibitisha kuwepo kwa Siasa zaidi nasio uzalendo ni baada ya Mhe. Waziri wa Elimu kusema kuwa sio kila tafiti inabaini ukweli na kusisitiza kuwa hata hoja ya Mhe. Mbatia imepitwa na wakati kulingana na muda ambao umetumika kuandaa tafiti ya hoja yake


Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Shukuru Kawambwa

Akiongea mbele ya Bunge Mhe. Shukuru Kawabwa ameponda juu ya kitabu kilichofanyiwa utafiti na kubaini mapungufu yaliyopo katika sekta ya elimu nchini tangu 1997





huku akifafanua mafanikio yaliyopatikana katika sekta ya Elimu nchini ikiwemo Sera ya Elimu inayotumika hadi hivi sasa

“ Utafiti uliofanywa kwa miaka 17 na Mheshimiwa Mbati yaweza kuwa kweli wakati mwingine yaweza kuwa ni uongo kwani sio kila tafiti inapata majibu ya kweli, akitaja maeneo ambayo yana vipengele vikuu vitatu juu ya mitaala, mutasari wa vitabu lakini hoja hizo zote” Alisema Mhe Kawambwa


EmoticonEmoticon