TANZANIA WAMFAGILIA MWAI KIBAKI, SASA OLD BAGAMOYO ROAD YAPEWA JINALAKE



 Barabara ya Old Bagamoyo imebadilishwa jina rasmi nakuitwa jina la Raisi wa Kenya anaye karibia kumaliza muda wake, Mwai Kibaki katika Uzinduzi uliofanywa na Rais Jakaya Kikwete akiwa pamoja na Raisi huyo mapema hii leo jijini Dar es salaam


Akiongea katika uzinduzi huo, Rais Mwai Kibaki amesema Tanzania iseme inataka nini kwa nchi hiyo, nakuongeza kuwa majina yanapokuwepo inamaana ya uhusiano mzuri kati ya nchi yetu na nchi hiyo ilikuweka kumbukumbu" Alisema Rais huyo


Barabara hiyo yenye urefu wa kilometa 10.1., ikitokea makutano ya Barabara ya Rashid Kawawa hadi njia panda ya Africana na kukutana na Bagamoro Road imebadilishwa jina na Raisi wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Jakaya Kikwete

Uzinduzi huo umefanyika Mbeye ya Waziri wa Ujenzi Prof. John Pombe Magufuli, Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Meck Sadic na Meya wamanispaa ya Kinondoni Mstahiki Yusuf Mwenda. Na Jina la barabara hiyo imetolewa kama Eshima kwa raisi huyo anaye karibia kumaliza mda wake

Raisi Mwaikibaki amebakiza muda wa wiki mbili ilikuachia ngazi ya Uraisi wa Kenya mara baada ya Uchaguzi mkuu wa nchi hiyo kufanyika March 4 mwaka huu.

Hatahivyo baadhi ya wakazi wa jiji la Dar es salaam, walikuwa na maoni tofauti juu ya uzinduzi huo huku wakihoji nikitugani hasa,


Raisi huyo wakenya ameifanyia Tanzania kiasi cha kumpa sifa ya jina la barabara nchini Mwetu

Iddi Abdala, amesema " Bado sijajua kwa nini Raisi nawatu wake wameamua kubadilijina, nikitugani hasa ameifanyia Tanzania kiasi cha kuweka kumbukumbu au kama kuna kitu kimefichwa basi tuambiwe" Alisema Iddi


" Barabara hii inahistoria ya watumwa ambao walikuwa wakipita kupelekwa Bagamoyo enzi hizo, kuiita Mwai Kibabi inafuta historia yake, kimsingi sijaona alichokifanya Rais huyo kwa Tanzania kiasi cha kupewa jina hilo" Alisema Idd

Naye Suza Lyimo. amesema Akuna shida jina lake kuwekwa ndani ya nchi yetu akielezea kwamba sisi ni Afrika Mashariki tukiwa na umoja siombaya japo naye akujua nikwanini imeamriwa hivyo.

Watu wengi amboa Blog hii imefanyanao mahojiano walipinga sana uamuzi huo huku wakijiuliza nikitugani alichokifanya Rais huyo nchini mwetu.

Picha kwa hisani ya Michuz na IPPMedia.com


EmoticonEmoticon