KUUNDWA TUME YA KUCHUNGUZA MATOKEO MABAYA KIDATO CHA NNE 2012, WAUNGWA MKONI, MPANGO WA SEDEP NAO WAGUSIWA


Kutokana na serikali kuunda tume ya kuchunguza matokeo mabaya ya kidato cha nne 2012, Profesa. Herne Joseph Mosha kutoka chuo kikuu cha Dar es salaam, Amesema kuwa serikali inaumuimu wa kuunda tume kuchunguza matokeo hayo ilikuweza kupata chanzo kimoja ambacho kinazungumzia chanzo cha matokeo hayo na nini chakufanya baada ya matokeo hayo mabaya kwani sivyema kuwatumia wanasiasa katika mambo ya kitaalam

Sivyema kuwatumia wanasiasa sana japo nao wanaumuimu, ilikupata mtummoja ambaye anatoa kiini cha tatizo nilazima tume iundwe kwani serikali aiwezi kutumia maoni yakila mtu, na pia serikali inayo haki ya kuunda tume na kwahilo sioni shida” alisema Prof. Herne Mosha

Jinsi ya kutekeleza mipango ya Elimu ndio bado aijaeleweka, Hakuna ambacho akijulikani na ninaamini hawatapata kitukipya ndani ya hii tume kwani tayari vilisha wekwa kwenye tafiti mbalimbali, sera na dira mbalimbali za elimu zilisema mipango mingi na changamoto nyingi ndani ya sekta ya Elimu, kushindwa kutekeleza ndio maana bado tunarudi nyuma, alisema Prof. Herne Mosha

Aidha Profesa Herne Mosha amesema kuwa kuna haja kwa serikali kuweka Sekta ya Elimu chini ya Wizara ya Elimu tu nasio ilivyo sasa ambapo sekta hiyo ikochini ya wizara ya elimu na tamisemi kituambacho kinapunguza uwajibikaji na kufanya wizara ya elimu kutokuwa na maamuzi yamwisho hasa kwa walimu namengineyo

Hakuna ambaye anaweza kumuwajibisha mwalimu akienda kinyume na mkataba wake, wala kufuatilia kwa umakini zaidi juu ya mambo fulnai kutokana na sekta ya Elimu kuwa ndani ya Tamisemi na wakati huohuo iko Wizara ya Elimu na mafunzo ya ufundi” Hapa napo paangaliwe, alisema Prof. Herne Mosha

Prof. Herne alisema kuwa, viashiria vya matokeo mabaya yalianza mwaka 2009 tangu serikali ilipoanza mpango wa maendeleo wa elimu ya secondary yani SEDEP ambao ulitaka kiasi cha ufaulu kianzie dara la I – III ambapo ni kwasilimia 32% mpaka asilimia 50% kwani takwimu zinaonyesha ndipo matokeo ya elimu yalipoanza kushuka. Profesa. Herne Joseph Mosha alisema

Hatahivyo, Prof Abdu Ntajuka Hamisi wa Lunga ya Kiswahili UDSM, amesema kuwa kuundwa kwa tume hiyo nimuhimu kwani tume inatoa matumaini ya kile walichokibaini kutokana na maoni ya watumbalimbali juu ya matokeo haya.

Tume italeta matokeo mazuri na yenye njia ya kufanya baada ya hili janga na kuganga yajayo, kwani nilazima wajue wanaanzia wapi, kwani awawezi kutoa msaada bila kuwa na data ya nini kifanyike” alisema Prof. Abdu Hamisi

Prof. Aliongeza kuwa, kufeli kwa wanafunzi kumanisha kilicho kusudiwa hakikufanikiwa, ama wanafunzi wamesomeshwa tofauti na mitaala, au vitabu walivyo someshwa sivyo na pengine watahiniwa awakuwa waangalifu kulinganisha masomo na mitihani

Kufeli kuna maana nyingi sana, pengine kuoanisha matokeo ya kuleta mafanikio kwenye ufaulu avikufikiwa kwani wameshindwa kufikia walicho kusudia' Alisema Prof. Abdu Hamisi

Naye mwalimu wa shule ya sekondari moja ya hapa jijini ambaye hakupenda jina lake litajwe alisisitiza kuwa serikali itegemee matokeo mabaya mwaka 2013 kwani msingi huu uliopo na ambao umewaangusha hawa waliopita bado upo na njia ya kutatua kwa sasa imechelewa, Alisema mwalimu huyo


EmoticonEmoticon