ASILIMIA 60 WALIOPATA SIFURI WAZIDI KUMLIZA MBATIA, ASISITIZA MITAALA NI TATIZO



Kushoto,Waziri wa Elimu Mhe.Shukuru Kawambwa, Kulia Naibu wake Mhe. Philip Mulugo


Kufuatia matokeo mabaya ya mitihani kidato cha nne 2012, Mwenyekiti wa chama cha NCCR Mageuzi na Mbunge wa kuteuliwa Mhe. James Mbatia amesikitishwa na kiwango hicho na kusema kuwa hali hiyo nikukosa usukani kwa elimu ya Tanzania.

Mbeshimiwa Mbatia amesema hayo hii leo ofisini kwake jiji Dar es salaam, akiongea na waandishi wa habari, ambapo alisisitiza elimu kuporomoka.
 
Elimu ya Tanzania inaporomoka kwa kukosa usukani na mwelekeo, kama maswala haya hayatachukuliwa maanani swala la elimu litaendelea kuwa kikwazo” Amesema Mbatia.

Akiongelea swala la wastani waufaulu ambapo asilimia 60 wamepata ziro (Divisio 0 ), asilimia 20 wamepata daraja la nne (Division IV), asilimia iliyobaki haiwezi kukuza elimya ya Tanzania na kwamba hali hiyo ni msiba kwa Taifa.

Mhe. Mbatia amesema, sababu inayosababisha hali hiyo ni mfumo mbovu usioeleweka wa Elimu pamoja na mitaala ya Elimu nchini ambayo inawaongoza wanafunzi juu ya Elimu yao, alisema.

Hakuna mitaala inayoeleweka ya elimu nchini, pamoja na iliyopo hivi sasa hii ndi inachangia elimu kuyumba, huku akiongea kwa masikitiko makubwa” alisema Mbatia.

James Mbatia kulia
 Aidha, Mbatia amesisitisa sana juu ya mitaala iliyowasilishwa Bungeni kikao kilicho pita na Waziri wa Elimu na mafunzo ya ufundi Mhe. Shukuru Kawambwa kuwa imechakachuliwa na sio halisi



 
Mitaala hii sio halisi huku akikionyesha kwa wanahabari, aina no. ya ISB, aina Nembo ya Taifa ya adam na hawa pamoja na saini hata ya mmiliki wake” alisema Mbatia

Matokeo ya kidato cha nne yalitangazwa jana na waziri wa elimu, huku wanafunzi Elfu 1641 tu ndio waliopata Division I, Elfu 6453 ndio wenye division II, Elfu 15,426 Division III, huku laki 103,327 wakipata Division IV na Laki 240,903 wakipata Division 0.


EmoticonEmoticon