ZOEZI LA KUONDOA WA HAMIAJI HARAMU HALINA UPENDELEO



Wizara ya mambo ya ndani nchini Tanzania imetoa ufafanuzi juu ya tuhuma kadhaa za uonevu na upendeleo, kuhusiana na zoezi linaloendelea hivi sasa la kuondoa wahamiaji haramu katika maeneo mbali mbali hapa nchini


Hii leo Blog hii ilishuhudia raia wa nchi mbalimbali miongoni mwao walikuwepo wamalawi zaidi ya 1500, wa Nigeria na nchi zingine wakijiandikisha katika ofisi za uhamiaji jijini Dar es salaam ili waweze kutambulika kisheria

Akiongea na thecampasvision Msemaji wa wizara ya mambo ya ndani ya nchi bwana Isaac Nantanga amesema zoezi hilo ni endelevu na kuwa sio la kibaguzi na rushwa kama ambavyo baadhi ya watu wamekuwa wakilalamika

Zoezi la wahamiaji harammu litakuwa endelevu hasa jijini Dar es salaam, huku maeneo ya pembezoni mwa nchi zoezi maalum litaendelea kwani maeneo hayo yanaongoza kwa kuwa na wahamiaji haramu.

Hapo jana baadhi ya wananchi kutoka kigoma na baadhi ya wabunge wao walikutana katika eneo la Tegeta kujadili suala hilo ambapo walidai kuwa zoezi hilo linafanywa kibaguzi na rushwa kitu ambacho wizara ya mambo ya ndani ya nchi imekikanusha.


EmoticonEmoticon