BAJETI YA WIZARA YA MAJI YA PIGWA CHINI, WABUNGE WAUNGANA – KILIO HAKUNA MAJI NCHINI, WAKATAA BILIONI 500 HAIWEZI KUTATUA TATIZO



KUTOKA BUNGENI



Hii itakuwa historia tangu Bunge hili kuanza, ambalo ni Bunge la 10 kikao cha13, baada ya Wabunge kuacha hitkadi za chama na kusimamia ukweli na hali alisi juu ya Tatizo la maji nchini
 

Hii leo Bungeni, Bajeti ya wizara ya Maji leo haijapitishwa na wabunge, kwakukataa kuunga mkono hoja mpaka njia madhubuti zitakapoletwa kwaajili ya tatizo hilo huku wakilalamika bajeti iliyotengwa ni ndogo kwa jinsi tatizo lilivyo

Wabunge walipaza sauti zao na kumtaka Waziri wa maji na umwagiliaji Mhe. Jumanne  Magembe ajipange nakuacha kuwasilisha hotuba yenye nyaraka za uongo kwao

"Wabunge wengi walisikika wakisema, takweimu hizi umetoa wapi, mara hili eneo halipo tanzania umelitoa wali.... nilazima tusimamie ukweli...siungi mkoni hoja" walimalizia

Wabunge hao ambao walikataa kuunga mkono hoja huku kila mtu akilia na kukosa maji jimboni mwake wakishangaa hotuba ya waziri ambao imeelezea miradi mingi iliyotekelezwa

Hatahivyo hoja hiyo haikupitishwa mpaka itakapo jadiliwa tena bungeni hapo na Mh-Spika wa Bunge Anne Makinda akalazimika kuahirisha bunge huku akiiagiza serikali ikae pamoja na kamati ya bajeti kutokana na kuonekana kuwa bajeti iliyotengwa mwaka huu ni ndogo na haitaweza kumaliza kelele za maji,hivyo kamati ya bajeti pamoja na serikali zikutane pamoja ili wajadili pesa hizo watazitoa wapi

Katika kipindi cha maswali ya papo kwa hapo kwa Waziri mkuu Bungeni, imebainika kwamba Tanzania ndio nchi inayoongoza kwa kuzalisha mkaa duniani kiasi ambacho kinatishia mazingira ya nchi yetu

"Waziri alijibu hali hiyo sinjema na isiendelee kwani inahatarisha rasilimali zetu, hivyo kuagiza swala hilo kushugulikiwa"

Tanzania ni moja kati ya nchi 10 zinazozalisha mkaa duniani huku asilimia 3 ya mkaa unaotumika duniani ukitoka Tanzania ambapo kwa siku Tanzania huzalisha Tani 2650 sawa na Tani milioni 10 kwa mwaka ,,,na hapo hapo mkaa huliingizia taifa dola milioni 650 (zaidi ya sh-bilioni moja )vile vile biashara hiyo inategemewa na familia zaidi ya milioni 1 nchini




EmoticonEmoticon