SIKU YA WAJASIRIAMAMLI DUNIANI- WASHAURIWA KUKOPA




Wajasiriamali wameshauriwa kutoogopa kukopa na kutumia taasisi za mikopo katika kuendeleza biashara zao

Hayo yamesemwa na Gershom Mpangala ambaye ni Meneja Masoko wa FINCA 



(FINCA Tanzania Limited) alipokuwa akifanya mahojiano na Blog hii. FINCA imekuwa ikitoa mikopo kwa wajasiriamali zaidi ya Elfu 70 hapa Tanzania

Mpangala amesema, swala la wajasiriamali wengi kuogopa kukopa ni moja ya kikwazo cha kutoendelea kwa biashara nyingi.

Aidha amewataka wajasiriamali kutambua kuwa hata wafanya biashara wakubwa au ambao wanamiliki biashara tofauti tofauti wamefanikiwa zaidi kwa kutumia mikopo kwenye biashara zao

“ Wajasiriamali wakubwa, mfano wanaofungua ma Benk na huduma nyingine kubwa katika jamii wame fanikiwa kutokana na kukopa, wakope au wahudhurie semina zinazo fundisha jinsi ya kuendeleza biashara kwakutumia mkopo, watafanikiwa zaidi” Alisema

Nidhamu ya Pesa, pia ni msingi wa kuendeleza biashara yako, ujue jinsi gani ya kupata Faida na kuokoa hela ya mtaji wako... hichi pia ni kikwazo kwani wengi hutumia faida anayo pata na mtaji bila kujua atumie pesa hipi katiya hizo ilikuendeleza biashara yake.

Ikiwa leo ni siku ya wajasiriamali Duniani, kwa Tanzania siku hii imeachwa kwenye mitandao kwani wajasiriamali wengi hawajui siku hii


EmoticonEmoticon