BAA LA NJAA KUTEKETEZA WATU ELFU 27 DODOMA, MBUGE AOMBA MSAADA

Mhe. John Nkamia kushoto wakati akiongea na Blog hii: Picha na campasvision.blogspot.com

Zaidi ya watu Elfu 27 Mkoani Singida wanaishi kwa kula Mizizi kutokana na ukosefu wa chakula tangu mwezi wa kumi na mbili mwaka jana, huku Serikali ikilifumbia macho swala hilo licha ya kuwa na taarifa hizo

Hayo yamesemwa na Mbunge wa Kondoa Kusini Mhe. Juma Nkamia alipoongea na Blog hii maeneo ya Bungeni Jijini Dar es salaam, Nkamia alielezea masikitiko yake kwa serikali kushindwa kutoa ufumbuzi licha ya kupewa taarifa kwa muda sasa

“Tatizo la wananchi wa singida kukosa chakula nila muda sasa, tayari nimetoa taarifa kwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda, Waziri wa Kilimo na Chakula Prof Jumanne Magembe lakini hakuna hatua yoyote iliyo fanywa kuwa nusuru wananchi na jaa kali” Alisema Nkamia

Jumla ya watu Elfu 27, kutoka tarafa za Kwa Mtoro, Farkwa, Goima na Mondo hawana chakula hivi sasa, Alisema Mbunge huyo na kuongeza kuwa taarifa amefikisha kwa wahusika wakuu pamoja na kumtaarifu mkurugenzi wa kitengo cha maafa katika ofisi ya Waziri Mkuu lakini hatua yoyote haijachukuliwa.

Mhe. John Nkamia, ameelezea kuwa angeweza angetatua tatizo hilo lakini inashindikana kutokana na idadi ya watu pamoja na mshahara wake hauwezi kutatua tatizo na kulimaliza kabisa hivyo kuililia Serikali kuokoa wakazi wa maeneo hayo na njaa hiyo.

Naiomba serikali isisubiri watu wapoteze maisha ndio waende kutoa msaada, kwani hali hii imetokana na kutopatikana na chakula cha kutosha katika msimu uliopita hivyo kuwalazimu wakazi wamaeneo hayo kukubwa na baa la njaa


EmoticonEmoticon