SIKU TANO NJE YA BUNGE MHE. LEMA AANGUKIA MIKONONI MWA JESHI LA POLISI



Askari wa Jeshi la Polisi wakilivuta gari la Mbunge Huyo juzi eneo la tukio Chuo cha AIA


Baada ya Mhe. Godbelss Lema kuhusishwa na vurugu za chuo chauhasibu Arusha ( Arusha Institute of Acountancy), hatimaye akamatwa na Jeshi la Polisi baada ya kibarua kizito cha kupiga kambi nyumbani kwake usiku kucha

Habari zilizo chapishwa na Tovuti ya chama hicho, zinadai kuwa Mbunge huyo hawezi kukamatwa mpaka pale Spika wa Bunge Mhe. Anna Makinda atakapotoa kibali cha yeye kukamatwa


Tarifa ambazo blog hii imefuatilia zina sema kuwa Lema tayari ametiwa mikononi mwa jeshi la polisi baada ya kukamatwa usiku wa manane nyumbani kawake ili kujibu tuhuma zinazo mkabili



Siku mbili zilizo pita Mhe Lema alikuwa kwenye umati wa wanafunzi wa chuo cha Uhasibu Arusha akiwatuliza hasira wakiwa na lengo la kuandamana kutokana na kifo cha mwanafunzi mwenzao Henry Koga ambaye aliuwawa kwa kuchomwa kisu na watu wasio julikana

Mbunge huyo pia anadaiwa kuchochea maandamano yaliyosababisha vurugu kiasi cha Mkuu wa Mkoa wa Arusha Magesa Mulongo kuzomewa na kupopolewa mawe na wanafunzi wa chuo hicho

Mhe. Lema alikwenda chuoni hapo ambapo nikaribu kabisa na nyumbani kwake kwa lengo la kutuliza gasia hizo, kitendo ambacho jeshi la polisi ilikiita cha uchochezi

VIDEO IKIONYESHA MHE. LEMA AKIONGEA NA WANAFUNZI KATIKA CHUO HICHO


Hatahivyo, Mhe. Godbless Lema ni miongoni mwa wabunge waliozuiliwa kuingia Bungeni kwa siku 5 baada ya kuhusishwa na vurugu zilizozuka Bungeni,

Mhe. Lema alizuiwa kuingia Bungeni kwakosa la kuwakataza askari kumkamata Mhe Tundu Lissu aliamriwa kutoka nje ya Bunge na Spika wabunge Mhe. Job Ndungai kwakosa la kuingilia hoja ya Mhe. Mwigulu Nchemba Wabunge wengine waliozuiwa ni Mhe. Tundu Lisu, Joseph Mbilinyi, Ezekiel Wenje na Peter Msigwa.

Lema hivi sasa anashikiliwa na Jeshi la Polisi Arusha akiusishwa na kuchochea vurugu za wanafunzi wa chuo hicho kuandamana, ambapo jeshi la polisi lilitumia mabomu ya machozi kuwatawanya wanafunzi hao


MKUU WA MKOA ARUSHA NAYE ALITINGA ENEO LA TUKIO KUTULIZA GASIA , NAHALI YA EWA IKACHAFUKA BAADA YA WANAFUNZI KUMZOMEA

                                                                                                              Hivi sasa chuo hicho kimefungwa kwa muda usiojulikana kutokana na matukio hayo ya uvunjifu wa amanai


EmoticonEmoticon