UHURU KENYATTA AAPISHWA KUWA RAIS WA AWAMU YA NNE-KENYA




Kenya imepata Raisi Mpya wa awamu ya Uhuru Kenyatta pamoja na Makamu wa Rais ambaye ni Willium Ruto, ambao wamechukua nafasi ya Rais Mwai Kibaki alie acha uongozi hii leo. Uhuru ameapishwa chini ya katiba ya nchi hiyo katika uwanja wa Moi Kasarani jijini Nairobi,

Wageni mashuhuri walihudhuria katika sherehe hizo, nipamoja na Rais wa Tanzania Mhe. Jakaya Kikwete na First Lady mama Salma Kikwete, Edward Lowasa na wengineo.Yoweri Kaguta Museven wa Uganda, Rais wa Sudan Kusini Salva kiir mayardit. Hatahivyo, Yoweri Museven ndiye aliye toa hotuba kwa niaba ya Wageni wote waalikwa kwenye sherehe hizo

Aidha Kenyatta ndiye rais mwenye umri mdogo zaidi kuwahi kuongoza nchi ya Kenya akiwa anaumri wa miaka 51 na ni mtoto wa rais wa kwanza wa Kenya Hayati Jomo Kenyatta. Hata hii leo aliapa kwa kutumia Biblia aliyotumia baba yake

Mpinzani mkuu wa Uhuru Kenyatta, Raila Odinga ambaye naye ni mtoto wa waziri mkuu wa kwanza wa nchi hiyo, hakuweza kuhudhuria sherehe hizo nayuko nchi AFRIKA KUSINI kwa mapumziko

Kenyatta na naibu wake William Ruto wanakabiliwa na kesi ya uhalifu dhidi ya binadamu katika mahakama ya uhalifu wa kivita ICC . Wanadaiwa kuwa washukiwa wakuu wa ghasia za baada ya uchaguzi mkuu uliofanyika miaka mwaka 2007.

Aliye kuwa mpinzania wake bwana Raila Odinga hakuhudhuria sherehe hizo na badala yake yuko nchini Afrika ya Kusini akila bata


EmoticonEmoticon