WANAFUNZI 35 VETA WALA SHAVU, KUTUMIWA NA NHC UJENZI WA NYUMBA ZA BEI NAFUU


Mashine ya hydraform kuzalisha matofali ya bei rahisi
Wanafunzi 35 kutoka chuo cha Fundi Stadi (VETA) wamechaguliwa kuendesha mashine ya Hydroform inayo fyatua matofali ya bei rahisi yatakayo tumiwa na shirika la nyumba la Taifa (NHC) katika ujenzi wa nyumba zaidi ya Elfu 5000 nchini 

wanafunzi 35 watakao hudhuria mafunzo hayo
Akiongea katika makubalianao na VETA yautoaji mafunzo kwa wanafunzi hao, Mkurugenzi mkuu wa NHC bwana Nehemia Kyando Mchechu amesema shirika hilo liko kwenye utekelezaji wa ujenzi wa nyumba Elfu 5000 za garama nafuu

“ MASHINE ya Hydroform itazalisha tofali nyingi kwa garama ndogo, pia aiharibu mazingira. Tutakamilisha ujenzi wa nyumba 5000 ambazo tutaziuza kwa garama za chini hivyo kila mtu ataweza kununua ”Alisema

Mkurugenzi mkuu wa NHC na Mkurugenzi mkuu wa VETA wakisaini makubaliano hayo

Mchechu amesema , NHC imejenga nyumba za Garama ya Millioni 35 tu lakini hizi sasa wanaitaji kupunguza garama hiyo, japo kuwa bei ya ujenzi wa nyumba inatofautiana mikoa hadi mkoa kulingana na upatikanaji wa maitaji ya ujenzi

Aidha Mkurugenzi Mkuu wa Chuo cha VETA bwana Zebedia Moshi amesema. Chuo hicho kimeanzisha mikakati ya kuwapatia ajira wanafunzi wanao soma chuo ni hapo ilikukabiliana na uhaba wa soko la ajira nchini kwani lengo lao nikufikisha asilimia 95% yawanafunzi wanao pata ajira ndani ya miaka 5
  
“ Ndai ya miaka 5 tunataka vijana wapate ajira kwa kiwango cha asilimia 95%, kwani hivi sasa ni asilimia 66% yawanafunzi wanaojiajiri kutoka vyuo vya VETA kote nchini huku Asilimia 43% wanahajiriwa, kwakushirikiana na wadau tutaongeza kiwango kilichopo hivi sasa” Aliseam

Jumla ya wanafunzi 35 ambao wamechaguliwa na NHC watapewa mafunzo ya wiki mbili baadae watagawanywa kwenye mikoa mbalimbali nchini ikiwemo GEITA, KIGOMA,SONGEA ,KATAVI TANGA na Dar es Salaam (Kigamboni)



EmoticonEmoticon