BILLIONI 20 KUENDELEZA WAFUGAJI WAGOGO WADOGO NCHINI

Serikali ya Tanzania imesema itahakikisha kwamba hakuna mtanzania ambaye atakufa kwa njaa mwaka huu licha ya kuripotiwa kwa baadhi ya maeneo yaliokumbwa na ukame na njaa kali

hayo yamesemwa na Waziri wa Uvuvi na maendeleo ya Mifugo Mhe. David Mathayo David hii leo jijini Da es Salaam, alipokuwa akifanya ufunguzi wa mradi wa uwezeshaji wakulima na wafugaji vijijini

Waziri Mathayo amesema, japo kuwa kuna uhaba wa chakula katika baadhi ya maeneo lakini serikali haita acha kuwafikishia chakula watu hao, na kuwa serikali inatambua maeneo ambayo yanasumbuliwa na njaa

Waziri Mathayo amezitaka taasisi binafsi kushirikiana na serikali ma maafisa ugani ili kuweza kufikia kilele cha mafanikio katika sekta ya kilimo na ufugaji.

Katika mradi huo kiasi cha Dola millioni 13.2 zimetolewa na UN ambayo ni sawa na Shilingi Billioni 20 za kitanzania ili kuwafanikisha wajasiliamali wadogowadogo kuendesha biashara zao pamoja na kutafuta masoko kwaajili ya bidhaa zao

Zaidi ya asilimia 75 ya watanzania wameajiriwa na kilimo, hivyo mradi huu utaleta maendeleo kwa watanzania kujiendeleza kiuchumi



EmoticonEmoticon