SERIKALI YAJIPANGA KUONGEZA MAPATO YA MADINI


Great Rift Valley Mining Summit (GRV) hii leo wamekutana nchini Tanzania kwa siku mbili kuangalia njia za kuongeza mapato kupitia vivutio vya madini

Mkutano huo umehusisha nchi zilizoko kwenye nchi za Bonde la ufa, miongoni mwa nchi hizo ni Uganda, Malawi, Zambia, Ethiopia, Mozambique, na Kenya

Akiongea kwenye mkutano huo, Naibu Waziri wa Nishati na Madini Mhe. Stephen Masele amesema Lengo kubwa la mkutano huo ni kuinua mapato yanayopatikana kwenye madini, pamoja na kuweka mazingira mazuri ya watanzania kuwekeza katika madini” alisema Masele

“Lengo kubwa ni kuainisha vivutio vya uwekezaji kwenye madini ilikuongeza mapato ya serikali” Alesema Masele


Aidha Masele amesema, tayari wameanzisha mfuko maalum wa kuudumia mazingira na watu wanao zunguka maeneo ya migodi ambayo inasaidia katika ujenzi wa mashule, barabara na Hospitali ikiwa pamoja na kutunza mazingira ya maeneo husika. Alisema

Naye Mtendaji mkuu wa mamlaka ya ukaguzi wa madini nchini (TMMA)
Bwana Paul Masanja amesema jumla ya shilingi Billioni 480 zimekusanywa na mamlaka hiyo kwa muda wa miaka 3 toka kwa makampuni makubwa ya madini nchini

“Jumla ya Billioni 480 zimekusanywa kwa miaka 3 toka makampuni makubwa nchini ambayo yanafanya biashara ya madini, kiasi hiki ni faida kwa taifa” na kuongeza kuwa kiasi hicho ni sawa na nusu ya faida ya asilimia 15.51% ya faida ambayo taifa inapata kulinganisha na wawekezaji.

Bwana Paul Masanja alisema kuwa, Tangu mwaka 1998 mpaka 2012 serikali imepata faida ya jumla ya shilingi Trillioni 12.6 ambayo nayo imekusanywa kwenye mapato ya migodi yote hapa nchini

Aliongeza kuwa, Kwa muda wa mwaka mmoja serikali inakusanya kiasi cha Billioni 1.4 kama makusanyo yatokananayo na madini ya ujenzi tofauti na ilivyo kuwa hapo awali, ambapo serikali ilikuwa inakusanya Millioni 3 tu kutoka kwenye madini hayo

Kamishna wa madini nchini bwana Ally Samaje amesema fursa za kumiliki hisa kwa watanzania ninyingi kuliko wageni kwani mtanzania anapaswa kuwa na hisa ya kiasi cha asilimia 25% zaidi ya wageni ili kuwawezesha kunufaika na madini hayo


EmoticonEmoticon