MALUMBANO YA KIDINI YATAWALA HOTUBA YA RAIS, AWATAKA WATANZANIA KUPENDA AMANI TULIYO NAYO



RAIS ALIA NA MGONGANO WA KIDINI NCHINI,   AGUSIA NYARAKA NA MATAMKO YANAYOTOLEWA , ASHANGAA KILA DINI KUILAUMU SERIKALI INAPENDELEA UPANDE MWINGINE, ASIHI WATANZANIA KUDUMISHA AMANI,UPENDO 




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dr Jakaya Kikwete amesema kuwa kitendo cha kila upande wa kidini kuilaumu serikali kuwa ina pendelea upande mwingine, sio kweli kwani serikali inajali dini zote. Rais amekuwa akihutubia taifa kila ifikapo mwisho wa mwezi katika hotuba ya mwezi huu mambo ya kidini yalichukua nafasi kubwa

Akiongea Ikulu Jijini Dar es salaam, Rais amewataka watanzania kuishi kwa upendo, umoja na mshikamano na kuachana na malumbano ya Kidini yanayoweza kupelekea uvunjifu wa amani ambayo ndio tunu ya taifa letu



“Kumekuwa na lawama kutoka kwa Waislamu kuwa serikali inapendelea Wakristo na nchi inaendeshwa kwa mfumo wa kikiristo,huku Wakristo nao Wakiilaumu serikali kuwa inawapendelea Waislamu na kutochukua hatua zozote zile pale makanisa yanapo chomwa kituambacho serikali inaangalia kwa kila upande bila kumpendelea mtu” AlihutubiaRais



Rais Kikwete amesema, Serikali iko dhabiti katika kulinda usalama wa Raia wake, Viongozi wakidini Mashehe pamoja na maaskofu, na malizake na kusisitiza kuwa sikweli kuwa serikali aichukui hatua zozote pale kunapotokea machafuko au uvunjifu wa amani unaohusiana na maswala ya kidini



“Kutokana na Kuchomwa kwa makanisa, kupigwa risasi na kujeruhiwa kwa viongozi mbalimbali wa kidini pamoja na mambo yanayoendana na hayo, Haimanishi Serikali imeshindwa kulinda watu wake au inamaanisha serikali aichukui hatua zozozote” Alihutubia Rais



Rais Kikwete amesema, Serikali imechukua hatua nakuwa tayari waliohusika wameshikiliwa, huku akieleza kuwa bado haija bainika moja kwa kama kama kuna kikundi kinacho husika na matukio yote, huku akisema kuwa bado uchunguzi wa kipolisi unaendelea ilikupata jibu sahihi



Aidha, aliongeza juu ya Nyaraka na Matamko mbalimbali yanayotolewa na viongozi wa Kidini kuwa yanaweza kupelekea hisia za machafuko na uvunjifu wa amani, na kuwaomba viongozi wa dini zote kuombea taifa liwe na amani. Pia amegusia swala la misikiti 3 jijini Dar es salaam kumuombea Itikafu ili afe ikiwemo Mkuu wa Majeshi nchini pamoja na Mkuu wa Kanda maalum ya Kipolisi ya Jijini Dar es salaam


RAIS JK AAGIZA WALIOHUSIKA NA UZEMBE WAKUBOMOKA JENGO LA GOGORA 16 WACHUKULIWE HATUA HARAKA

Katika Hotuba hiyo Rais alizitaka mamlaka husika kuwachukulia hatua za haraka wale wote waliohusika na uzembe na kupelekea jengo la gorofa 16 kuporomoja na kusababisha vifo vya watu 30 huku wengie 17 wakinusurika kifo,



Rais amesema kuwa kutokana na hali ya eneo la tukio nidhahiri kuwa hali hiyo ingeweza kuzuilika huku akizitaka mamlaka zinazo husika kuweka njia za kuzuia matukio kama yaho yasiweze kutokea tena, na kuagiza hatua za kisheria zichukuliwe didhi yawale wote waliohusika na uzembe huo



Hatahivyo Rais alitoa shukrani kwa Jeshi la Polisi, vikundi mbalimbali pamoja na watu waliojitolea kuhakikisha kuwa wana wafukua waliofukiwa kwenye kifusi cha jengo hilo ikiwa ni pamoja na kuwapa pole wawewote walifiwa na ndugu na jamaa zao

RAIS ATOA WITO KWA WAANDISHI WA HABARI

Akiongea katika hotuba yake, Rais amewataka waandishi wa habari kutoandika habari ambayo inalenga kuchochea vurugu za kidini kwani kutofanya hivyo kunaweza kupelekea kupotea kwa amani ya nchini yetu na kutolea nchi jirani ambazo tayari zimewaikukumbwa na machafuko



Aidha amewataka wamiliki wa vyombo vya habari kutoruhusu mtu kutoa habari inayolenga kukyza tofauti za kidini nakuomba ushirikiano nao katika kukemea na kuelimisha jamii juu ya tofauti zao ili pasiwepo na tofauti hizo


EmoticonEmoticon