Prof. Ibrahim Lipumba amewataka watanzania kutunza muungano na kuachana na mawazo ya kuuvunja muungano licha ya matatizo yaliyopo.

Prof. Lipumba ame yasema hayo hii leo jijini Dar es salaam, alipokuwa akiongea na vyomba vya habari,



katika makao makuu ya chama hicho.ambapo amesema tuangalie zaidi juu ya kushugulikia matatizo ilikudumisha muungano kwa maendeleo ya wote

“Watanzania wengi wanaangalia juu ya changa moto zilizopo na badala ya kushugulikia matatizo yaliyopo ilikuweza kusonga mbele kama taifa” Alisema Lipumba

Nikweli kuna matatizo ya muungano, hata mimi ninayajua lakini hayo hayawezi kutufanya kuuvunja muungano, bali tujikite kwenye njia ambazo zitatuwezesha kuujenga muungano huo. Alisema

Kesho maadhimisho ya muungano yatafanyika jijini Dar es salaam, ambapo viongozi wa juu watahudhuria sherehe hizo, ikiwa ni miaka 49 ya muungano

Aidha kutokana na vurugu zilizo vuka huko Liwale mkoani Lindi, Prof. Lipumba amewataka wakazi wa maeneo hayo kuachana na maandamano na kuishauri serikali kukubali kukaa chini na wakazi hao kujadili juu ya swala hilo

Hapo jana vurugu vilizuka miongoni mwa wakulima na vyama vya sushirika vya Korosho mkoani Lindi baada ya kutoafikiana juu ya bei halali ya kununulia bidhaa hizo

Prof. Lipumba ameitaka serikali kuwalipa fedha wakulima hao kama walivyo ahidiana kwenye kikao cha mauzo kilicho fanyika mwaka 2012

“Wananchi wali kabidhiwa Tsh. 200/= kwa kilo badala ya shilingi 600/= kama ilivyo ahidiwa na kukubaliwa kwenye mkataba wa mauzo, serikali nilazima iwalipe wakulima kulingana na walivyokubaliana” Alisema

Serikali ifanye utafiti juu ya swala hili, na kuunda chama cha wakulima wenyewe kuuza korosho hizo hili haya yasijirudie. Alisema

Prof. Lipumba pia aliongelea swala la matusi bungeni na kuwataka wabunge kuwa tambua watanzania walio wachagua kuwa hawa vutiwi na hali hiyo hivyo kuacha mara moja.


EmoticonEmoticon