TUME YAUNDWA KUCHUNGUZA MADUDU BANDARINI, NI KAMATI YA BUNGE YA HESABU ZA SERIKALI

Kamati ya Bunge ya Hesabu za serikali hii leo, imeunda tume ya watu watatu ili kuchunguza sababu za kutokuwepo kwa mtambo wa kupimia mafuta bandarini yani Flow Metre, ambayo haipo bandarini hapo tangu Februari mwaka 2011 hali inayo ipotezea serikali mapato

 

Akiongea na waandishi wa Habari baada ya kikao kilicho husisha wadau kutoka Bandarini TPA, TRA na Wakala wa Vipimo Tanzania,




Mhe. Zitto Kabwe ambaye ni Mwenyekiti wa kamati hiyo amesema Kamati yake imefikia uamuzi huo baada ya kuona kuna mvutano juu ya kutokuwepo kwa Flow Metre bandarini

“Mvutano uliopo kati ya TPA, TRA na Wakala wa vipimo Tanzania, Kamati itaunda tume yawatu watatu nikiwemo mimi, ilikufanya uchunguzi juu ya hasara inayotokana na kutokuwepo kwa mtambo huu ambao unaijulisha Serikali nikiasi gani cha mafuta kimeingia nchini ” Alisema Zitto


Katika kikao hicho mvutano mkali ulikuwepo katiya TPA na Wakala wa Vipimo Tanzania ambapo Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Vipimo Tanzania Bi. Magdalena Chuwa na Alekzander Ndibalema kutoka TPA walikuwa wakivutana juu ya kutokuwepo kwa mzani huo wakupima mafuta Bandarini

Picha zote na thecampasvision
“ Bi Magdalena Chuwa alidai mtambo huo uliharibika nakuwa wamepata malalamiko toka kwa wadau mbalimbali, naye Alekzander Ndibalema akidai kuwa mtambo huo aujaharibika” kila mtu alimtupia lawama mamlaka nyingine juu ya kuharibika kwa mtambo huo

Mtambo wa kupimia mafuta bandarini Flow Matre ulinunuliwa tangu mwaka 2004 hadi kuharibika mwaka 2011, kituambacho kimesababisha mafuta kuingia bandarini Tanzania bila kuwepo na uhakika wa kiasi gani cha mafuta kimeingia kutokana na kutokuwepo kwa mtambo huo wa kupima mafuta.


EmoticonEmoticon