MIKATABA FEKI YAMLIZA JAJI WEREMA, RASILIMALI KUTONUFAISHA WATANZANIA NAKO KWA MKERA, AWATAKA WANASHERIA KUPITIA MIKATABA UPYA


Jaji mkuu Frederick Werema amewataka wanasheria kuondoa malalamiko ya watanzania juu ya mikataba mibovu kwa kupitia upya mikataba ambayo imeshapitishwa ili kuokoa rasilimali za Taifa

Hayo yamesemwa leo jijini Dar es salaam na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema alipokuwa akifungua mafunzo ya sheria ya makubaliano ya kibiashara kwa wanasheria 40 wa Serikali.



Jaji Werema amesema, wanasheria nilazima waamuke na kuomba kuipitia upya mikata upya na waangalie niwapi walikosea ilikuifanya kazi yao kuwa ya weledi na tija kwa taifa.

“Kama sisi tusipo sema wanachi watasema, waandishi kupitia makala na magazeti watasema, nilazima tuseme penye mapungufu bila kumuogopa mtu” alisisitiza Jaji Werema




Jaji Werema alisisitiza kuwa mengi ya tokea yakuibiwa rasilimali zetu yanasababishwa na makosa ya sheria, hivyo tuamke kwani maendeleo ya watanzania yako mikononi mwetu. Alisema kwa msisitizo

“Tuwalinde watanzania na mikataba mibovu (FEKI)tunayo simamia kama wanasheria .. makosa kama ya IPTL, DOWANSA nanyingine yasiwepo kwani makosa mengi yakuibiwa yanasababishwa na makosa ya kisheria” alisema




Pia amewataka wanasheria kujifunza lunga mbalimbali ilikuweza kukabiliana na wawekezaji mbalimbali kwani hiyo itawasaidia kuwa na uwezo mkubwa wakuchambua sheria mbalimbali huku akisisitiza juu ya sheria ya – Tanzania Investment Act[CAP 38 R.E 2012]

Aidha amesema, watanzania wengi hawajui kuwa watungasheria ni wabunge ambao huruhusu mikataba inayo walinda wawekezaji hivyo kuwataka wanasheria kuiwasimamia.




Mafunzo kwa wanasheria hao 40 itafanyika kwa wiki moja lengo ikiwa ni kuwafundisha juu ya kuingia makubaliano ya mikataba ya kibiashara. Mpango uliofadhiliwa na UNDP. Mafunzo hayo yatafanyika shule ya sheria (Law School of Tanzania)

kwamuda mrefu sasa nchi imekuwa ikipoteza rasilimali zake kutokana na mikataba mibovu inayopitishwa na viongozi pamoja na wanasheria.


EmoticonEmoticon