MITAA 3 MANISPA YA KINONDONI YA KOSA WAJUMBE WA MABARAZA YA KATIBA, KISA ITKADI ZA KISIASA

Mwenyekiti wa mtaa wa 


Kata 3 katika Manispaa ya Kinondoni zimeshindwa kupata wa wakilishi wao katika Mabaraza ya katiba ya Wilaya kwa kile kilicho daiwa kuwa ni itkadi za kisiasa

Akiongea na Blog hii kwanjia ya simu, Msemaji wa manispaa ya Kionondoni Bwana. Sebastian Mhowera amesema kata hizo zimeahirisha wenyewe uchaguzi huo hivyo hazita kuwa na wawakilishi wake katika Baraza la wilaya kwani siku iliyo teuliwa kwa shuguli iyo tayari imemalizika.

Zoezi kwa manispaa ya Kinondoni imekamilika isipokuwa kata 3 zimeshindwa kufanya uchaguzi, wanaichukulia zoezi hili kama nila kisiasa jambo ambalo haliusiani na zoezi la leo, Alisema Mhowera

Mhowera alitaja kata hizo kuwa ni Kata ya Alimauwa A - Mtaa wa Kijitonyama, Kata ya Kisiwani – Mtaa wa Makumbusho pamoja na Kata ya Mburahati – Mtaa wa barafu., ambazo zimeshindwa kufanya uchaguzi huo

Aidha Blog hii ilifanya mahojianao na Mwenyekiti wa mtaa wa Mzimuni kata ya Makumbusho  Bwana Abdi Alyy, ambaye amesema katika kata yake waliomba wananchi 72 huku wakiudhuria watu 80 katika uchaguzi huo

Watu wengi waliomba lakini tume wachagua 8 tu kulingana na utaratibu ulivyo wekwa, zoezi lilikuwa salama na haki nawanachi wamechagua wenyewe walio waitaji na mimi nitawakilisha majina yao” alisema Bwana Ally

Ally, aliwashukuru wakazi wakata yake kwa kujitokeza kwa wingi katika uchaguzi huo hali iliyopelekea kusiwepo na malalamiko yoyote wala changa moto kwenye uchaguzi huo

Mchakato wa kuandaa katiba mpya unaendelea, na hivi sasa imemalizika hatua ya kutafuta wajumbe wa mabaraza ya katika ya kila mtaa ambao utaunda mabaraza ya katiba ya wilaya, ambapo watawakilisha wananchi wengine katika ukusanywaji wa maoni ya katika mpya ambapo Wajumbe hao ni 8 kutoka kila mtaa kama ilivyo tolewa na Jukwaa la katiba nchini 


EmoticonEmoticon