SHULE MAALUM ZA WALEMAVU ZAGEUKA KAMBI, WAZAZI WAKWEPA KUWACHUKUA KIPINDI CHA LIKIZO




Mwenyekiti wa Chama Walemavu wa Ngozi Nchini bwana Erenest kimaya
amewaomba wasamaria wema kupeleka msaada wa hali na mali katika shule maalum kwa ajili ya Albino ilikuwawezesha wanafunzi wa shule hizo kupata maitaji yao yakila siku wawapo shuleni

Akiongea na thecampasvision, bwana Erenest amesema wanafunzi wa shule za Buhangija na Mitindo zilizopo Mwanza na Shinyanga wengi wao hawakuenda likizo kama inavyo takiwa kuwa nakujikuta wanakaa kambi kwa muda wote walikizo wa mwezi wa 12, kutokana na wazazi wao kutowachukua shuleni hapo, kitu ambacho kinapelekea kuwa na mahitaji mengi kutokana na kuvunjika kwa utaratibu wakila siku.

Bwana Erenest amesema, Serikali inautaratibu wa kutoa msaada kipindi cha masomo inapofikia likizo na wanafunzi wanakuwa wapo shuleni kuna kuwa na tabu kidogo, nakuwaomba wasamaria wema kuwakumbuka wanafunzi hao

" Baadhi ya wanafunzi awakuendalikizo kwaiyo maitaji yanaongezeka, ila wangeenda likizo maitaji yahapa napale yangekuwepo kulingana na mpango wa serikali wa kutoa maitaji katika shule hizi" Alisema Erenest

Aidha Aliwataka wazazi kuwapenda watoto wenye uleavu wa ngozi na kuwachukua katika shule zao inapofika siku za likizo kwani kuwa telekeza mashuleni kunawanyima haki zao za msingi na kujumuhika na wazazi wao kama ilivyokawaida kwa watoto wengine

" Wazazi wengi wamewaacha watoto wao shuleni kipindi cha likizo, kwa madai ya usalama kituambacho nikama kisingizio kwani wengi wamepata sababu za kuwambali nao, tunawaomba wasifanye hivyo" Alisema Erenest

Elimu inahitajika kwa wazazi ambao bado wanakwepa swala la walemavu wangozi, kuwapa elimu kutaleta ushirikiano kati yetu na wazazi wao kwenye swala la zima la Usalama, alisema Erenest nakuongeza kuwa mpango wa kuwaeleimisha wakazi wa shinyanga juu ya kuwapenda watoto wao utafuata baada ya muda mfupi kuanzia sasa

Zaidi ya Wanafunzi 50 hawakuweza kwenda likizo katika kipindi cha mwisho wa mwaka kutokana na kutochukuliwa na wazazi wao huku wengine wakihofia usalama wao, shule hizo ni Mitindo Mwanza pamoja na Buhangija Shinyangaambazo zote zinasomewa na wanafunzi wenye ulemavu wa ngozi-Albino


EmoticonEmoticon