KIWANGO CHA UFAULU FORM II CHAPANDA, MAMIA WAFELI NA WENGINE KUFUTIWA MITIHANI


Wizara ya elimu na mafunzo ya ufundi nchini Tanzania leo imetoa matokeo ya mtihani wa kidato cha pili uliofanywa mwaka jana 2012ambapo wanafunzi lakimoja elfu thelathini na sita 136.000 watalazimika kurudia kidato cha pili, huku wengine 23 wakifutiwa matokeo yao


Akiongea na waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam, Naibu waziri wa Wizara hiyo mheshimiwa Philip Mulugo amesema
wanafunzi walio feli watalazimika kurudia kidato cha pili, licha ya kiwango cha ufaulu kupanda kwa asilimia 19.15 ikilinganishwa na matokeo ya mwaka jana


Waziri amesema, Serikali imefuta matokeo ya wanafunzi 23 kutokana na vitendo vya udanganyifu. Waziri ameongeza kuwa kiwango cha ufaulu kwa mikoa ya kusini yani Lindi na Mtwara ni mabaya kutokana na shule zilizofanya vibaya kutoka katika mikoa hiyo


Mwaka jana, wanafunzi wa kidato cha pili walishangaza pale baahi yao walipo chora Mpira, Mistari ya Muziki na kudanganya katika mitihani yao


EmoticonEmoticon