SERIKALI KUONGEZA DAWA ZA MAGONJWA NYEMELEZI YA UKIMWI

WAZIRI WA AFYA NA USTAWI WA JAMII MHE.
WIZARA ya Afya na Ustawi wa Jamii kupitia mpango wa Taifa wa kudhibiti Ukimwi NACP, imetenga fungu maalum kwaajili ya kununulia Dawa za kudhibiti magonjwa nyemelezi ya ugonjwa huo ilikukabiliana na uhaba wa Dawa na Vifaa tiba katika vituo vyote vya umma

Akiongea leo Bungeni leo wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum Mhe. Magreth Mkanga, Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Mhe. Dr Hussein Mwinyi amesema Serikali itahakikisha kuwa dawa hizo zinapatikana kwa wingi katika vituo vya Afya ili kudhibiti uhaba wa Dawa hizo za magonjwa nyemelezi

Aidha Dawa kama za Kifua kikuu, Kisonono na Malaria zinapatikana Bure Bila malipo kwa watu wenye Virusi vya Ukimwi katika vituo vyote vya kutolea huduma za Afya za umma na baadhi ya vituo Binafsi ambavyo vimeidhinishwa na Wizara hiyo


EmoticonEmoticon