WANAFUNZI IFM WAKANUSHA KUCHUKUA WAKE ZA WATU KIGAMBONI

Raisi wa wanafunzi- Michael Charles aliyovaa skafu, pamoja na wanafunzi wengine wa IFM

Raisi wa Serikali ya Wanafunzi IFM (IFMSO) Michael Charles amekanusha wanafunzi wa IFM kutembea na wake za watu huko Kigamboni na kuahidi kulifanyia uchunguzi jambo hilo ilikubaini ukweli wa shutuma hizo kama zinahusiana na tukio la kulawitiwa kwa wenzao wawili pamoja na kuporwa kwa vifaa vyao

“Nimara yangu ya kwanza kusikia tuhuma hizi, na tunafanya uchunguzi ilikujua undani wa tukio hili. Tayari tumeweka watu ambao wataleta majibu iwapo kama kuna wanafunzi wanaovuta Bangi, Wanaojiusisha na Ulevi na iwapo kuna yeyote yuko kwenye makundi ya uhalifu, na ripoti hiyo itatolewa kwenye Bunge la Wanafunzi” Alisema Charles

Akiongea na Blog hii, Michael Charles amesema, hakuwai kusikia tuhuma hizo kabla ya tukio lililotokea Taree 10. January 2013, lakulawitiwa na kuporwa mali kwa wenzao wawili ambao wanaishi katika Hostel Binafsi (Off Campas) huko maeneo ya Uwanja wa Machavi- Kigamboni.

Tukio hilo lilisababisha Wanafunzi wa chuo hicho kuandamana ilikushunikiza vyombo vya usalama kuingilia kati na kuchukua hatua juu ya matukio ambao yamekuwa yakihatarisha usalama wao katika Hostel wanazo panga huko maeneo ya Kigamboni. Wanafunzi hao wamedai kuibiwa Laptop zaidi ya 100 pamoja na kulawitiwa kwa wenzao wawili

Wanafunzi wa chuo cha IFM juzi waliandamana hadi makao makuu ya Jeshi la Polisi (WIZARA YA MAMBO YA NDANI) wakimtaka Kamanda wa Kanda maalum ya Mkoa wa Dar es salaam bwana Suleiman Kova kujitokeza na kusikiliza madai yao, ambapo Waliahidiwa uhakika wa usalama wao na malizao


EmoticonEmoticon