ZAIDI YA MIAKA 20-25 TANZANIA KUPATA MEDALI KWENYE MICHUANO YA OLYMPIC
Filbert Bayi, alipokuwa akiongea na Campus Vision leo

Kutokana na kutokuwepo kwa mfumo mzuri wa michezo mashuleni Itaigarimu Tanzania miaka 20 mpaka 25, kupata timu bora itakayo iwakilisha katika michuoano ya Olympic kulingana na jitihada zilizopo hivi sasa

Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu wa Kamati ya Olympic Tanzania (T.O.C) bwana Filbert Bay akiongea na Campas Vision hii leo jijini Dar es Salaam, Bayi ambaye ameshinda tena kitihicho kwa awamu nyingine, amesema Michezo mashuleni ndio itakayo leta matokeo mazuri ya michezo nchini

“Kutokana na kuvurugika kwa michezo ya Umitashumta, Sekondari kwa takriban miaka 15 hivi sasa, na kwa jitihada zinazo chukuliwa hivi sasa miaka 20-25 ndio tutafanikiwa kupata timu itakayo iwakilisha Tanzania Vizuri katika michuano ya Olympic”Alisema Bayi

Bayi alisema, Ni muhimu kugawana jukumu la kuinua michezo miongoni mwa wadau wote, ambao ni Mashuleni,Vyama vya Michezo na Wachezaji ikiwa ni pamoja na Serikali kwa ujumla, nakuwataka watu wanao laumu bila kutoa mchango wowote kutofanya hivyo

“Nirahisi sana watu kutoa lawama pindi timu inaposhindwa, lakini hakuna anaye toa mchango na kujitolea kuwasaidia katika mambo mbalimbali ambayo nayo yanakwamisha na kupelekea kutopata Medali au kutofika mbali kimichezo”. Alisema Bayi

Hatahivyo Bayi alitoa wito kwa Serikali kuzisapoti shule binafsi zinazoonyesha uwezo wa kuinua michezo na kuwataka baadhi ya Viongozi kuacha kuzirudisha nyuma na kuzipondea shule hizo, kwani mfumo mzuri wa Michezo utapatikana kwa kukazania michezo mashuleni


EmoticonEmoticon