VYUO VIKUU VYATAKIWA KUREKEBISHA KASORO ZAO KWA WAKATI

Tume ya vyuo vikuu Tanzania TCU, imetoa wito kwa Wanafunzi na Menejmenti ya vyuo vyote nchini kuchukua hatua kurekebisha kasoro mbalimbali zinazojitokeza vyuoni mwao kwa wakati ilikudhibiti madhara yanayoweza kujitokeza

Wito huo umetolewa, baada ya Tume hiyo kuingilia kati mgogoro ulidumu kwa wiki tatu katika chuo kikuu cha kimataifa cha Kampala, na kubaini matatizo ya uongzi wa chuo hicho na kuutaka uongozi wa chuo hicho kushugulikia matatizo hayo

Madai ya wanafunzi hao nipamoja na, Ada na malipo mengine, kukosekana kwa kitabu cha matarajio(Prospectus), Huduma za maktaba, Huduma za Intanet, Mfumo wa mitihani ya marudio, Sifa ya utafiti na maandiko kwa wanafunzi wa mwaka wa tatu, Sifa ya walimu, Serikali ya wanafunzi na katiba yake,Uwakilishi wa wanafunzi kwenye kamati na vyombo mbalimbali vya chuo,

Malalamiko mengine ni, Ufundishaji katika Shahada za udaktari wa binadamu na uhandii, Wanafunzi wa Kitanzania kufikiriwa kulipa ada ya chini kuliko wageni, Ratiba za vipindi pamoja waalimu kuwa na vipindi vingi,Kitengo cha Udhibiti wa ubora cha chuo(KIU Quality Assurance Unit), mahafali na miadhara ya kielimu, Matokeo kutolewa kwa wakati kupitia mtandao,.

Utaratibu wa wanafunzi wenye sifa za Diploma kujiunga na Kozi mbalimbali za ngazi ya Shahada,na malipo wakati wa kujiandikisha chuoni, ni maeneo ambayo yanaitajika kutolewa ufumbuzi. na makubaliano yaliyofikiwa nikuwa matatizo yote yatatuliwe 


EmoticonEmoticon