WATANZANIA WAKO MILLIONI 44.9, JK ATANGAZA LEO UWANJA WA MNAZI MMOJA JIJINI DAR ES SALAAM



RAIS Jakaya Kikwete ametangaza idadi ya watanzania ambapo amesema kwamba jumla ya watanzania 44929002 ambao ni sawa na (44.9)milioni, huku akisema kwamba idadi ya watanzania wote wanaoishi Tanzania Bara ni 43625434 na visiwa vya Zanzibar na Unguja ni 1303568.

Idadi ya Watanzania wote ni Millioni 44 929 002, ambayo ni sawa na milioni 44.9, matokeo hayo yametajwa na RAISI wa Jamuuri ya muungano wa Tanzania JAKAYA KIKWETE, katika uzindizi wa matokeo ya Sensa 2012. 

Aidha Tanzania bara inajumla ya watu Milioni 43.625.434, huku Tanzania Visiwani Zanzibar kuna watu Milioni 1.303.568. Idadi ya watanzani ainaongezeka kwa kasi ndani ya miaka 10 ambayo watu huesabiwa

Sensa ya Kwanza Tanzania ilianza mwaka 1967 mara baada ya Uhuru, ikifuatiwa na mwaka 1978, 1988, 2002 na 2012, Zoezi la Kuesabu watu nchini hufanyika kila baada ya Miaka 10


EmoticonEmoticon