JAMII YATAKIWA KUONDOA VIKWAZO KWA   WALEMAVU

Mwenye kiti wa chama cha Walemavu wa Ngozi Nchini,Bwana Ernest Kimario ameitaka jamii kutochukulia siku ya Walemavu kuwa kama siku ya Harusi ya mtu binafsi, na badala yake jamii nzima ijumuike pamoja ilikuondoa vikwazo vinavyo wakabili walemavu.

Bwana Ernest Amesema, kila mtu Anatakiwa kujiuliza nikikwazo gani ambacho anamuwekea Albino au Mlemavu yeyote, akashindwa kushiriki kama watu wengine...kwani kauli mbiu ya Mwaka huu inasema Ondoa Vikwazo Tujenge Jamii Shirikishi kwa Wote.
Sawala la Walemavu kutopata elimu,ajira na fursa zingine katika jamii nikikwazo, kwaiyo jamii shirikishi inaitajika ilikuondoa vikwazo kwa walemavu

Hatahivyo bwana Ernest Amesema, Mauaji na Unyanyapaa kwa walemavu wa ngozi Albino, umepungua hasa katika seemu za vijijini, na kwamba waiomba serikali kutoa vifaa ambavyo vitawawezesha walemavu kuweza kusoma kwa amani


EmoticonEmoticon