KAULI ZA MAGUFULI YAZIDI KUPIGIWA KELELE

Chama cha upinzani nchini Tanzania cha Chadema, kimeitaka serikali kufafanua
kauli aliyoitoa waziri wa ujenzi, Mheshimiwa Dkt John Pombe Magufuli,
alipoalikwa kwenye mkutano wa kampeni za chama cha ODM 
cha nchini Kenya kama ni ya serikali au yake mwenyewe.

Waziri kivuli wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa, Mbunge wa 
Nyamagana mhe. Hezekiah Wenje, amesema hayo leo kufuatia kile alichodai 
kuwa nihatua ya Tanzania kuingilia siasa za ndani za Kenya.
Wenje ameongezea kuwa endapo matatizo yatatokea kauli ya Mheshimiwa
huyo itakuwa imeleta tafsiri mbaya miongoni mwa wakenya

Kwa mujibu wa Wenje, chama hicho kimepokea malalamiko mengi kutoka
kwa Watanzaniawanaoishi Kenya kuwa huenda wakapata matatizo 
endapo kutatokea kutoelewana baina ya pande hasimu 
katika siasa za nchi hiyo hasa kipindi hiki nchi hiyo inapoelekea
kwenye uchaguzi mkuu. 
 
nikukumbushe mpenzi msomaji juu ya habari hiyo
ambayo pia iliandikwa the blog hii ya Campas Vision
taree 7.12.2012

 MAGUFULI NA KAMPENI ZA KENYA, ATUA NAIROBI KUMUUNGA MKONO RAILA KUELEKEA UCHAGUZI MKUU WA NCHINI HUMO

 
 Waziriwa Miundombinu Mhe. John Pombe Magufuli leo yuko Nchini Kenya ambapo 
amehudhuria kampeni za uchaguzi zinazo endelea jijini Nairobi, Akiwa 
anatoa sapoti kwa Waziri Mkuu wa Nchi hiyo Mhe. Raila Odinga anaye gombe
 nafasi ya Urais



Raila Odinga ambaye ameungana na mwana 
siasa maarufu Kalonzo Musioka nakuanzisha chama chama cha OrangeNDC, 
ilikukabiliana na Wahasimu wao Uhuru Kenyata naWilium Ruto ambao nao 
wameungana, uchaguzi Mkuu wa Kenya unatabiriwa kuwa na Upinzani mkubwa 
kutokana na mabadiliko ya kisiasa yanayoendelea nchini humo



Aidha, Uchaguzi utafanyika ifikapo March
 mwakani. huku kukiwa na kesi kwa baadhi ya Viongozi ambao wanagombea 
nafasi ya Urais, katika mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu wa Kivita ICC .
          



 baadhi ya Tweets za leo za Viongozi hao








Kama unavyo onekana ni tweet za viongozi hao, pia Waziri Mkuu wa Zimbabwe Morgan Tsvangirai ameudhuria kampeni hizo

updates. 

Magufuli asema, Raila anahofu ya Mungu na anafaa kuiongoza Kenya nakuweka msisitizo wa wananchi wa nchi hiyo kumpigia kura kiongozi huyo


 


EmoticonEmoticon