WASANIFU MAJENGO WAJIPANGA KUWAPORA KAZI WACHINA, WADAI RUSHWA NIKIKWAZO KWAO

Serikali imetakiwa kuweka sheria za majenzi ili kuweza kuwadhibiti na kuwachukulia hatua wanao kiuka taratibu za kujenga kwani mpaka sasa hakuna sheria inayowatia hatiani hata pale inapotokea jengo limebomoka na kusababisha madhara kwa jamii.


Tume shuhudia jengo lime bomoka hivi karibuni lakini ningumu kuchukua hatua za kisheria juu ya wahusika kwakuwa sheria ya kuwatia hatia ahipo, hivyo serikali ilishugulikie hili swala na tunaliomba Bunge kuangalia zaidi”amesema Hussein

Ameongea hayo wakati akifanya mahojiano na waandishi wa habari katika mkutano uliowakutanisha wasanifu majengo wa Afrika mashariki kwa lengo la kujadili ni jinsi gani wataweza kutumia fedha zao kuendeleza vyuo vinavyotoa taaluma ya majengo katika nchi za ukanda huo, Rais wa chama cha Wasanifu majengo Tanzania Arch. Husein Igangula amesema watatumia fedha zao kuendeleza taaluma hiyo.


Tangu Jumuiya hii ianzishwe nimiaka mingi sasa na tumeona kuwa fedha nyingi tulizonazo benki zitumike kuendeleza vyuo vinavyo fundisha taaluma hiyo ikiwa pamoja na wale wanafunzi wanao chukua somo hilo ilikuweza kupata wafanisi zaidi”Amesema Hussein

Tunataka kulinda rasilimali zetu na fedha tulizo nazo, ilitupate mbinu za kushindana na wachina ambao kwa kiasi kikubwa ndio wanaotumiwa na nchini mwetu katika kufanya ujenzi mbalimbali.

Mbinu za kushindana na wachina nipamoja na kuongeza ufanisi wetu kupitia elimu na teknoligia za kisasa, na kwakweli hapa nchini kuna wasomi sio kwamba hawapo kuwatumia wachina kila mara katika kazi ambazo hata wazawa wanaziweza ndicho tunacho pambana nacho hivi sasa”amesema Hussein.


Aidha ameitaka serikali kuwatumia wazawa katika kazi zake nakusisitiza kuwa kazi zaio zinagarimu pesa nyingi hivyo mianya ya rushwa inaweza ikawepo hivyo watanzania pia waondokane na swala hilo ilikuweza kuwainua wasanifu majengo wandani.

Naye Arch Kaisi Kalaamboambaye alikuwepo kwa niaba ya Raisi wa Jumuhiya hiyo barani Afrika amesema ni vyema wananchi wakajenga tabia ya kuwatumia wasanifu majengo katika ujenzi wao bila kuhofia garama kwani wao wapo kwaajili ya watu wote.

Wanaojenga nyumba ndogo pia wanahitaji wasanifu wasihofie garama kwani kila garama ipo kwaajili ya kazi husika, nyumba ikiwa ndogo garama pia nindogo hivyo wasiogope”amesema Kaisi.

Mkutano huo wasikimbili umewakutanisha wasanifu majengo ukada wa afrika mashariki na hutamalizika hapo kesho jijini Dar es salaam.



EmoticonEmoticon