MAKAMBA AOMBA SERIKALI IAONDOWE VIKWAZO VIJANA




Serikali imetakiwa kuhakikisha vijana wanapewa ewezo wa kutumia vipaji vyao kujiajiri na kuajiri wengine kwa kuwaondolea vikwazo vinavyo wakabili bindi wanapo taka kuanzisha biashara au kupata mkopo katika mabenki hapa nchini.




Hayo yamesemwa jijini Dar es salaam na Mhe. January Makamba wakati wa uzinduzi wa tuzo za vijana chini ya miaka 30, ambapo Mhe. Makamba amesea, kujituma na kutumia fursa kwa vijana inategemeana na vikazo mbavyo kuna muda wanakumbana navyo na kuitaka serikali kuondoa vikwazo hivyo



kijana anataka kusajili biashara yake lakini kuna mlolongo mrefu sana ambao unafanya anakata tamaa, au anahitaji mkopo benki lakini wanahitaji hati ya nyumba huyu kijana anatoa wapi nyumba? Sasa kama serikali ikiangalia hivi nadhani vijana wataweza kuonyesha uwezo wao”Alisema Makamba


Aidha, alisema Mfumo wa elimu wa nchi yetu nao urekebishwe iwe elimu ambayo itawapa vijana uwezo wa kutatua matatizo yanayo mkabili, kushirikiana na wengine na sio elimu tu ambao bado itamfunga kuendana na dunia ya sasa. Alisema




Mhe. Makamba amesema katika Bunge lijalo Serikali imeandaa muswada ambao utawasilishwa juu ya kuwepo kwa Baraza la Vijana kwaajili ya kushugulikia matatizo ya vijana kama ajira, elimu na baraza hilo liwepo kisheria ili liweze kuwa na nguvu

baadhi yetu tumekuwa tukipenda bara hili lianzishwe haraka kwani litao tao majibu kwa matatizo ya vijana na serikali imejipanga vyema kuhakikisha kuwa bunge lijalo tunajadili nini cha kufanya” Alisema





Naye Mkurugenzi mkuu wa Youth for Africa bwana Awadhi Malasi amesema Taasisi yake inawakumbuka sana vijana kutokana na mchango wao katika jamii hivyo tuzo hizo zitawapa motisha vijana wengine kufanya vyema zaidi. Amesema

Awadhi amesema hii ni mara ya kwanza kwa taasisi hiyo kutoa tuzo hizo hapa nchini lakini kila mwaka kutakuwa na mabadiliko juu ya tuzo hizo kwani hata mikoani na watapewa fursa ya kushiriki




Kwa kupata washindi katika tuzo hizo unapiga kura kupitia mtandao wao ambao ni 
http://www.youthawards.or.tz  au kwa njia ya simu andika YOA acha nafasi kisha tuma kwenda 15584. Tuzo zitatolewa tarehe 17/8/2013.


EmoticonEmoticon