JESHI LA POLISI LA KANUSHA KUMLENGA MNYIKA NA BOMU, WAKAMATA KIWANDA CHA SILAHA DAR, NA MAJAMBAZI SUGU 8

Picha hii ahiusiani na habari hii


Jeshi la Polisi kanda maalum ya Dar es salaam, hii leo limekanusha tuhuma kuwa Bomu lililo lipuka katika mkutano wa Chadema uliofanyika kwenye viwanja vya Sahara Mabibo siku ya Jumamosi tarehe 21/07/2013 halikuwa limemlenga Mhe. John Mnyika ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Ubungo kama taarifa za awali zilivyo eleza

Akiongea na waandishi wa habari jijini Dar es salaam, Kaimu Kamanda wa Polisi kanda maalum ya Dar es salaam DCP Ally Mlege amesema taarifa zimekuwa zikipotoshwa juu ya tukio hilo, lakini ukweli ni kuwa bomu hilo lililipuka kwa bahati mbaya na hakuna mtu yeyote aliye jeruhiwa

Bomu hilo lililipuka kwa bahati mbaya baada ya Askari no. E.5340 D/CPL JULIUS ambaye alikuwa ndani ya gari la Polisi lenye namba PT 1902 alipokuwa anasogeza Box lenye mabomu ya mamchozi ya kurusha kwa mkono ndipo Bomu hilo likalipuka.

Hatahivyo Chadema hawakuruhusiwa kufanya mkutano eneo hilo lakini baadae waliondoka kwa amani katika eneo hilo bila madhara yeyote kujitokeza na kuamia katika maeneo ya Ubungo na kumalizia mkutano wao. Amesema DCP Ally Mlege


KARAKANA YA KUZALISHA SILAHA MAENEO YA 

KAWE MZIMUNI, NA MAJAMBAZI 8 WANASWA NA 

RISASI 56


Majambazi 8 wamekamatwa na Polisi wa kanda maalum ya Dar es salaam, wakiwa na silaha 5 pamoja na kiwanda cha kienyeji cha kutengenezea silaha na vifaa mbalimbali vya kufanyia uhalifu maeneo ya Kawe Mzimuni, kiwanda hicho kilikuwa chini ya Charles Francis Masunzu mkazi wa eneo hilo

wengine ni Matula Rashid dereva pikipiki mkazi wa mbezi, Omary Hassan kinyozi mkazi wa Mabibo, Mardha Muhagama mkazi wa Mbezi Kibanda cha mkaa na Mwasiti Maulidi mkazi wa mbezi msumi, watuhumiwa walikuwa na SMG yenye usajili no.02704 ikiwa imekatwa kitako na risasi 20 ndani yake.

Bunduki hiyo SGM no.02704 aliporwa Askari Polisi Wilaya ya Rufiji akiwa anasindikiza magari toka ikwiriri mkoani pwani mwaka 2007, majambazi hayo wametumia silaha hiyo kwa takribani miaka 7.

Aidha baada Charles Francis Masunzu mkazi wa mzimuni baada ya kufanyiwa upekuzi alikutwa na Shortgun moja no. 2539 double bore, Reffile 3 iliyo sajiliwa kwa no. TZ CAR 42871, Reffile 3 iliyosajiliwa kwa no. CAR83744,Reffile 3 ikiwa imefutwa namba, Pistol KJW Works, pamoja na mitutu 5, pingu,risasi 36 na maganda 17 ya risasi, mkebe wa Short gun, funguo mbali mbali, misumeno ya vyuma na vielelezo zingine vingi vinavyo husiana na uhalifu

Pia katika msako mwingine maeneo ya Kijitonyama Polisi walikamata Maragi ya wizi 5 Engine 3 za magari, vipande vya magari yaliyo katwa huku wezi 5 wamagari wakitiwa nguvuni.

Wahusika katika uhalifu huo ni Godlove Damasi, Anna Kway, Sharif Ahamad, Salehe Abdala Ally, pamoja na Nassoro Mohamed


EmoticonEmoticon