UNYAMA NCHINI: KWA MUDA WA MIEZI 6 VITENDO VYA UBAKAJI VIMEFIKIA ELFU 2965, WATOTO 394 WAMELAWITIWA HUKU WATOTO 127 NAO WAKITUPWA


Picha ya mtoto aliye zikwa akiwa hai mbeya na baba yake, hapo ni baada ya kufukuliwa na polisi

Haki ya kuishi kwa watanzania imeendelea kukiukwa katika kipindi cha miezi sita iliyopita kupitia matukio mbalimbali yaliyo kinyume na haki za binadamu ikiwa ni pamoja na Polisi kuua raia, polisi kuuawa mikononi mwa raia, mauaji ya alibino, mauaji ya vikongwe kwa imani za kishirikina, wananchi kuvamia vituo vya polisi, vitendo vya ubakaji.


Hayo yameelezwa katika taarifa ya hali ya haki za binadamu nchini katika kipindi cha kuanzia January hadi June mwaka huu iliyotolewa leo na kituo cha sheria na haki za binadamu ambayo pia inaonesha kuongezeka kwa vitendo vya ukiukwaji wa haki za binadamu vitendo ambavyo vinatokana na wananchi kujichukulia sheria mkononi.


Mtafiti kutoka kituo hicho Bwana Pasience Mlowe ndiye aliyesoma taarifa hiyo mbele ya waandishi wa habari hii leo jijini Dar es salaam ambapo amesema kuwa elimu ya kutosha juu ya haki za binadamu itolewe kwa wananchi ili kuzuia vifo visivyo vya lazima hapa nchini


Katika kipindi cha January hadi june mwaka huu Jumla ya askari polisi 8 wameuawa na wananchi, raia 22 wameuawa chini ya vyombo vya ulinzi, watoto 127 wametupwa, watoto 394 wamelatiwa, vifo 597 vimetokana na raia kujichukulia sheria mkononi, vifo 303 vimetokana na imani ya kishirikina na vitendo 2965 vya ubakaji vimeripotiwa.


Katika matukio ya kubakwa huko ukerewe mwanza mwanaume wa miaka 40 aliyejulikana kwa jina la Emanuel Halala alimbaka mara mbili mtoto wa miaka 8, huku mtoto wa miaka 3 aliye bakwa na mwanaume wa miaka 30 huko mkoani Mbeya matukio ambayo yanazidi kila ripo zinavyo zidi kutolewa


Aidha kuna mtoto aliye zikwa akiwa hai na baba yake huko Mkoani Mbeya kwa madai ya kuachana na mama yake mtoto huyo alikuwa wa miaka 4, lakini katika matukio mengi hakuna hatua zozote za kisheria zilizo chukuliwa didhi ya wahusiaka wa matukio hayo. 

Shirika hili limeitaka serikali kuendesha kampeni juu ya elimu ya haki za binadamu kama ambavyo wamefaulu katika maleria na ukimwi ilikuondoa matendo ya ukatili na unyanyasaji katika jamii ya watanzania.


EmoticonEmoticon