MIILI 7 YA WANAJESHI WALIO UWAWA DARFUR KUWASILI NCHINI HAPO KESHO

Miili ya wanajeshi 7 waliofariki huko nchini Sudan - Darfur huenda ikawasili hapo kesho baada ya kupewa heshima za mwisho na majeshi yanayolinda amani nchini humo hii leo

Habari zilizo andikwa na mtandao wa UNAMID zinasema tayari miili hiyo imeagwa tangu majira ya mchana na kuanza safari ya kuletwa nchini kwa mazishi








Hatahivyo taarifa ambazo hazijathibitishwa na Blog hii kwani jitihada za kuwasiliana na msemaji wa jeshi ziligonga mwamba baada ya kutopewa ushirikiano wa kutosha na simu kuita bila kupokelewa

Taarifa zinasema kati ya wanajeshi 14 waliokuwa mahututi 4 tayari wamefariki Dunia....... Blog hii itakujuza zaidi kadri habari zitakavyo kuwa zinatufikia      = Picha kwa hisani ya Michuzi Blog


EmoticonEmoticon