VIJANA WALILIA KUTOPEWA BARAZA LAO, KUJADILI RASIMU YA KATIBA

  



Vijana wote nchini wametakiwa kujiunga bila kujali itikadi zao ili kuweza kupigia kelele kuwepo kwa baraza la taifa la vijana litakalo jadili mambo ya Rasimu ya kuundwa kwa katiba mpya hapa nchini

Akiongea na waandishi wa habari hii leo jijini Dar es salaam, mwenye kiti wa jukwaa la vijana Tanzania bwana Fahami Matsawilly amesema kuwa tunaomba ibara ya 43 itamke wazi kuwa kila kijana anao wajibu wa kushiriki shuguli za kijamii na maendeleo kwa ujumla

“Vijana wote tunaombwa kuungana bila kujali itikadi zetu za kisiasa, kidini, kabila na elimu ili kuweza kutetea changa moto zinazo tukabili hapa nchini

Hayo yote yamekuja baada ya JUVITA kubaini kuwa matatizo yanayowakabili vijana kama Ukosefu wa ajira, makundi kama yale ya Machinga, dereva wa bodaboda na vijana wanao fanya kazi majumbani na makundi mengine ni lazima wawe na chombo kitakacho wa wakilisha kwenye vyombo vya maamuzi ya katiba mpya

Pia amewataka vijana kupeleka mapendekezo yao kwa wawakilishi wa mabaraza ya katiba ili ibara ya 43 iweze kufanyiwa marekebisho

“Cha ajabu baraza la taifa la vijana halimo kwenye rasimu ya katiba mpya, wakati nchi nyingi zenya mabara za ya taifa ya vijana, kwa nini Tanzania hiyo nafasio hakuna” Alisema

Baadhi ya nchi ambazo zina baraza la vijana linaloshigulikia matatizo ya vijana ni pamoja na Costasica, Slovenia, Rwanda , Uganda pamoja na Kenya na nchi zingine nyingi

Uundwaji wa Katiba mpya umefikia katika hatua za mabara ya Rasimu ya katiba mpya ambapo mabaraza hayo yataanza kukaa kuanzia Ijumaa ya wiki hii tarehe 12.


EmoticonEmoticon