DAR ES SALAAM IS BUSY AS OBAMA, BUSH AND OTHER PRESIDENTS VISIT TANZANIA


Mchaka mchaka unaendelea kwa viongozi wa juu, vyombo vya uasala pamoja na wananchi kwa ujumla kutokana na ujio wa marais wengi kwa kipindi cha wiki mbili Mfululizo

Ikumbukwe hapo wiki jana kulikuwa na mkutano wa Smart Pertnership International Dialogie 2013 hapa nchini mkutano ulijumuisha marais wapatao 9, mkutano huo umemalizika hii leo jijini Dar es salaam

Hii leo tena tumeshuhudia ugeni mkubwa wa Barack Obama na mkewe Michell Obama pamoja na Familia yeke, wakati huo huo hapo kesho tutapata ugeni wa Rais mstaafu George W Bush pamoja na mkewe Bi Laura

Viongozi hao wa marekani hapo kesho watakuwa na shuguli nyingi Obama akitakiwa kushiriki matukio 10 huku Michell na Laura wakiwa na mazungumzo na Wake wa marais wa barabi Afrika na mwenyeji wao Mama Salma Kikwete lengo ikiwa ni kuinua wanawake nchini

Katika matukio yatakayo hudhuriwa na Obama hapo kesho, ni  Uzinduzi wa mpango wa Simbioni utakao fanyika katika kituo kikuu cha kuzalishia umeme cha Ubungo, pia ataweka Shada la maua katika ubalozi wa marekani ikiwa ni kumbukumbu ya watu waliouwawa katika shambulizi la kigaidi la bomu mwaka 1988 huku Dar es salaam pamoja na kutembelea kituo cha watoto wa mitaani.


Wananchi wanatakiwa kuamka asubuhi na mapema ili kuepuka adha itakayo tokana na barabara kufungwa  kwa muda ilikupisha shuguli zitakazo fanywa na raisi huyo kumalizika kwa wakati

Barabara zitakazo fungwa ni Barabara ya Nyerere kuanzia saa 3 hadi saa 5 asubuhi, Barabara ya Ali Hassan Mwinyi, Sam Nujoma na barabara ya Morogoro, Nelson Mandela ambayo ataitumia wakati akiondoka hapo kesho kurejea marekani

Hatahivyo kutakuwa na vikundi, burudani na tarumbeta vitakuwa vimejipanga pembeni mwa barabara ya Kipawa, Jet Club, Vingunguti, Tazara, Kamata, Rwele Gerezani na Posta ya zamani eneo la Azania Front kumlaki Rais huyo wa marekani 

Ongeza kichwa


EmoticonEmoticon