KAMPUNI YA PROACTIVE YAJIPANGA KUWAAJIRI WAZAWA KATIKA MIRADI YA GESI LINDI NA MTWARA

Wadau mbali mbali wanao jishugulisha na shuguli za uchimbaji mafuta na gesi katika mkoa wa Lindi na Mtwara, hasa kampuni ya Proactive Solutions ambao wamejipanga kuwapa elimu vijana wa Lindi na Mtwara jinsi ya kufanya kazi katika makampuni ya kuchimba gesi


Wakazi wa Proactive Sulution akiwa kwenye banda lao. Loveness Nathan na Novatus Mango.


Akiongea na Blog hii hapo jana Mkurugenzi mtendaji wa kampuni

Proactive Solutions bwana  Nestory Phoye amesema kampuni ya 

ke itatoa elimu kwa vijana wa mtwara ili waweze kufanya kazi

katika makampuni mbalimbali kwani bila kupata elimu hiyo 

kufanya kazi itakuwa tabu.



Shughuli za uchimbaji na uzalishaji wa Gesi na mafuta katika mikoa ya Lindi na Mtwara utagharimu kiasi cha Dola 60 za kimarekani, ambayo ni sawa na zaidi ya shilingi Bilioni 97 za kitanzania.


Wadau hao wamejadili njia za kutumia ili kuweza kuwahusisha wazawa katika miradi yao na jinsi ya kupata eneo la kufanyia shughuli zao za uchimbaji wa gesi katika mikoa hiyo.


Corporate sales manager bi Jamila Holaki akitoa maelekezo ya bidhaa zao katika mkutano wa wadau wa Gesi na Mafuta

Akiongea na waandishi wa habari katika mkutano huo, Mkurugenzi
 Mkuu wa TPDC Bwana Yona Kilaghane amesema kuwa lengo lao
 kubwa ni kuwashirikisha wazawa katika shughuli zote za uzalishaji
 na kuongeza kuwa gesi itasindikwa katika mikoa hiyo ya Lindi na 
Mtwara.


Mkutano huo ulioanza leo na kumalizika kesho jijini Dar Es Salaam utafungwa na Waziri wa Nishati na Madini Mhe. Sospeter Muhongo.




EmoticonEmoticon