SHILINGI BILLIONI 160 KUKUSANYWA KWA MWAKA KUPITIA TOZO ZA LAINI YA SIMU YA KILA MWEZI

Photo: HOTMIX (11:00 Jioni): Leo ni siku ya ongezeko la watu duniani, Je idadi kubwa ya watu inachangia vipi maendeleo ya Taifa?

Serikali yasisitiza kuanza kukata kodi ya Tshs 1000 kwa kila laini ya simu, yasema inahitaji kukusanya bilioni 160, Je hii ina athari gani kwa watumiaji wa simu?

Ndani ya studio tutakuwa mastaa wa movie na music, pia utapata nafasi ya kuliona gari lililobuniwa na watanzania na kutengenezwa na watanzania, unadhani mwendo-kasi wa gari hili utakuwa ni kilomita ngapi kwa saa?

Pamoja na story kibao za leo, studio tutakuwa na Selemani Zedi mbunge wa Bukene mkoani Tabora, mtupie swali lolote hapa naye atakujibu.


>TOZO YA LAINI KWA MWEZI WABUNGE NDIO WALIPITISHA
>YADAIWA ITAPATIA NCHI BILIONI 160
>BILIONI 231 NAZO ZATOLEWA NA SEEDEN, 
>NA ADB BANK YAIKOPEHA TANZANIA BILIONI 286

Serikali imeendelea  kusisitiza kodi ya Line za simu ambayo itakatwa kila mwezi kwa watumiaji wa simu nchini

Akijibu swali lililo ulizwa na mmoja wawaandishi wa habari katika mkutano wa kusaini mkataba na nchi ya Sweeden, Waziri wa Fedha Dr. William Mgimwa amesema serikali ili chukua uamuzi huo baada ya wabunge ambao ni wa wakilishi wa wananchi Bungeni kukubali kupitisha Bungeni swala hilo

“Wananchi wana lalamika lakini wawakilishi wao ambao ni wabunge ndio walipitisha aina hii ya tozo hivyo serikali inajipanga kuanza mchakato wa kupata fedha hizo ili kuweza kuongeza kipato”Alisema

Aidha Dr. Mgimwa amesema kuwa serikali itapokea shilingi Billioni 160 kwa mwaka kutokana na kukata tozo hizo”Amesema

Akitoa ufafanuzi wa matumizi ya fedha hizo Dr. Mgimwa amesema kuwa fedha hizo zitatumika katika kusaidia maitaji ya jamii kama vile Hospitali, mashule na barabara”Alisema Dr. Mgimwa

Hii inamaana kama kila mwaka mmiliki wa line moja atatozwa shilingi Elfu 12 hali ni tete kwa wale wanao miliki laini zaidi ya Mbili.

Tozo hiyo itaanza kukatwa rasmi kuanzia Julai 2013 mwezi huu

Wananchi wengi wamezidi kulalamikia tozo hizo huku baadhi ya wabunge nao wakidai kuwa swala la laini za simu aikuwekwa Bungeni kujadiliwa kwa wazi 

BILLIONI 231 KUTOKA SWEEDEN KUENDELEZA MITAMBO YA UMEME NA UCHUMI

Serikali ya Tanzania imepokea shilingi bilioni 231 kutoka serikali ya Sweden kwa ajili ya kuendeleza miradi mbalimbali nchini

Waziri wa Fedha Dr. William Mgimwa amefafanua kuwa  mikataba miwili iliyotiwa saini leo ni kwa ajili ya matumizi tofauti ambapo mkataba wa kwanza wa shilingi bilioni 202 unalenga kuongeza nguvu katika kuhamasisha ukuaji wa uchumi na kupunguza umaskini

Mkataba wa pili wa jumla ya shilingi bilioni 129 utaelekezwa katika shughuli za ukarabati wa mitambo ya kuzalisha umeme iliyopo Hare jijini Tanga, nakuongeza megawati 21 katika umeme wa taifa

“Hivi sasa hare inazalisha megawati zisizo zidi tisa 9, nakuwa serikali imeamua kuongeza uzalishaji wake kwani kuna upatikanaji wa maji ya kutosha katika eneo hilo” amesema.

Dr. Mgimwa amesema, Hii ni sehemu ya jitihada za serikali kufanyia kazi vipaumbele vya mwaka huu wa fedha 2013/2014 ambapo kipaumbele cha kwanza ni miundombinu ya Nishati ya umeme na barabara.

Serikali ya Sweden imekuwa mstari wa mbele miongoni mwa washirika wa maendeleo nchini kusaidia ukuaji wa sekta ya nishati hususani Umeme hapa nchini

BARABARA YA ARUSHA-HOLILI KUJENGWA AUGUST 2013 MAPAKA DEC 2018

Barabara ya Arusha-Holili mpaka Taveta na Voi nchini Kenya inatarajiwa kuanza ujenzi wa kupanua barabara hiyo baada ya Tanzania kusaini mkataba wa mkopo wa shilingi Billioni 286 kutoka Banki ya maendeleo Afrika AFDB

Akiongea na waandishi wa Habari hii leo jijini Dar es salaam, Waziri wa Fedha Mhe. Willium Mgimwa amesema kuwa ujenzi wa barabara hiyo yenye urefu wa kilometa 42, utaanza August mwaka huu na kumalizika December 2018.

Aidha, Mradi wa ujenzi wa barabara hiyo itasaidia usafiri wa watu zaidi ya Laki 5 na 84 kwa upande wa Tanzania ikiwa pamoja na kurahisisha usafiri kwa watalii watakao tembelea mkoa wa Arusha na Kilimanjaro

Tanzania itarudisha mkopo huo baada ya Miaka 40 lakini mda wa kuanza kulipa mkopo huo ni miaka 5 ijayo, katika kurudisha fedha hizo Tanzania itatoa Asilimia 4.7 huku Kenya ikitoa Asilimia 5.9.


EmoticonEmoticon